2014-05-30 09:38:09

Maaskofu wa Afrika Kusini watoa msaada kwa jumuiya inayoteseka machimboni


(Vatican Radio) Baraza la Maaskofu la Afrika Kusini, limetoa kiasi cha Rand 75,000, kwa jimbo la Rustenburg Afrika Kusini kusaidia maelfu ya watu wanaoishi katika mazingira magumu na walioathirika na mgomo katika machimbo ya platinum.

Migomo, huu ulioingia katika wiki 18, ni muda mrefu zaidi na wenye vurugu zaidi katika historia ya migodi ya Afrika Kusini. Mgodi huo wa platinum unamilikiwa na Kampuni ya Anglo American Platinum, Impala Platinum na Lonmin inayopambana na upinzani kutoka Chama cha Muungano wa wafanya kazi na wajenzi machimboni.


mgomo huu , unazidi kusukuma shimoni uchumi wa taifa, na pia ghasia dhidi ya wale wasiotaka kugoma tangu mwanzo na kusababisha watu kadha kupoteza maisha na una shamirisha hali mbaya ya kibinadamu katika jamii ya madini na katika makazi ya jirani ambapo watu , wengi wao wakiwa ni walioathirika na virusi vya ukimwi, na pia wanakufa kwa uhaba wa chakula .

Askofu Kevin Dowling wajimbo la Rustenburg, Kevin Dowling , ambaye anaendesha hospitali kubwa ya ( Tapologo ), vituo vya huduma , jikoni supu , kliniki na vituo vya kurefusha maisha, anajitahidi kusaidia wachimba madini hao na jamii iliyo kata tamaa Rustenburg.

Akizungumza na Linda Bordoni wa Radio Vatican alisema, serikali kupitia waziri wake mpya kwa ajili ya madini, imeahidi kuingilia kati mazungumzo kati ya Muungano wa wafanyakazi katika migodi na wamiliki wa migodi hiyo .








All the contents on this site are copyrighted ©.