Wito kwa Boko Haramu: Fuateni njia ya mazungumzo, upendo na kuepuka chuki.
Askofu Mkuu Mstaafu wa Douala , Kardinali Tumi Wiyghan , ametoa wito kwa Boko Haramu,
kuwaachie huru bila masharti, Mapadre wawili wamisionari, wa Shirika la Italia la
Fidei Donum wa jimbo la Vicenza, Padre Giampaolo Gian na Padre Antonio Allegri , pamoja
na Sista Martha, Mkanada, waliotekwa nyara katika eneo la Kaskazini mwa Nigeria kati
ya 4 na Aprili 5 katika Jimbo la Maroua - Mokolo kaskazini mwa Cameroon. Kardinali
Tumi ametoa wito huo kwavyombo vya habari na kupitia Shirika la habari la FIDES, ambamo
amewaomba mashabiki wa kikundi cha boko haramu kuwachia wamisionari hayo bila masharti.
Kardinali amesisitiza na kulaani akisema kwamba ghasia haiwezi kutatua kitu chochote,
bali mamlaka ya Boko Haram, ikubali kufuata njia ya mazungumzo, upendo na kuepuka
chuki kwani kuna faida zaidi.