Wakati huu waamini wengi kutoka ndani na nje ya Uganda wanapoelekea Namgongo kwa ajili
ya maadhimisho ya Siku kuu ya Mashahidi wa Uganda inayofanyika kila mwaka ifikapo
tarehe 3 Juni, Vikosi vya ulinzi na usalama nchini Uganda vinaendelea kujiimarishwa
ili kukabiliana na uwezekano wa mashambulizi ya kigaidi nchini humo kama inavyotokea
kwa nchi jirani ya Kenya.
Ubalozi wa Marekani nchini Uganda umetoa onyo hilo
na kusema kwamba, Marekani inasikitishwa na vitendo vya kigaidi vinavyoendelea kujitokeza
nchini Kenya kiasi cha kuwajengea watu hofu na mashaka kuhusu usalama wa maisha na
mali zao.