2014-05-29 10:24:13

Cor Unum Mwenyeji wa Mkutano wa Mashirika ya Katoliki ya Hisani Syria


Vatican Radio) Siku ya Ijumaa, Mei 30, Baraza la Kipapa " Cor Unum " litakuwa mwenyeji wa mkutano wa uratibu wa Mashirika Katoliki ya Hisani , yanayo fanya kazi katika mazingira ya mgogoro wa kisiasa Siria.

Mkutano huo, unajumuisha mashirika 25 yanayo fanya kazi Syria na Mashariki ya Kati, unafanyika katika muundo wa awamu mbili, Wakati wa asubuhi , baada ya kuwasilishwa na Kardinali Robert Sarah , Rais wa Cor Unum , ambaye ndiye mratibu mkuu wa kazi za Mkutano huo, kutafuatia taarifa kutoka kwa Katibu wa Nchi wa Vatican , Kardinali Pietro Parolin .

Wasemaji ni pamoja na Askofu Mkuu Mario Zenari , Mjumbe wa Kitume wa Papa nchini Syria, na Askofu Antoine Audo , Rais wa Caritas Syria. Na hatimaye, mkutano utatazama taarifa za ofisi ya kazi zilizofanyika katika Beirut, zilizo anzishwa mwaka jana, kwa ajili ya kukusanya na kusambaza takwimu juu ya kazi za mashirika Katoliki. Wakati wa Mchana mkutano utatazama masuala ya utendaji wenye ushirikiano kati ya taasisi na vyama mbalimbali Syria na nchi jirani.


Lengo la mkutano linakwenda sambasamba na njia zilizochukuliwa miaka miwili iliyopita na Jimbo la Papa , na kama matokeo yake Mkutano wa Juni 4-5 , 2013 , ulioandaliwa na Baraza la Kipapa , kwa ajili ya kutathmini kazi zilizo kwisha fanywa na Mashirika Katoliki ya hisani katika mazingira ya mgogoro wa vita vya Syria ,kwa kuzingatia hali halisi na utambuzi wa vipaumbele kwa siku zijazo. Syria ni kiini cha tahadhari ya jumuiya ya kimataifa, kutokana na mwendelezo wa kipeo cha ubinadamu katika mgogoro wake kama matokeo ya vita.








All the contents on this site are copyrighted ©.