Kama kawaida ya kila Jumatano , Papa akiwa Vatican , alitoa Katekesi yake kwa mahujaji
na wageni waliokuwa wamekusanyika katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro.
Katika Katekesi hii , ametaja hasa nia za kufanya hija katika Nchi Takatifu ,
aliyokamilisha siku ya Jumatatu, akieleza kwamba, hija hii imekuwa ni zawadi kubwa
kwa Kanisa, na hivyo anamtolea Mungu shukurani. Kwa majaliwa ya Mungu, aliweza kuitembelea
nchi hii iliyobarikiwa , yenye kuwa na matukio ya kihistoria ya Ukombozi ulioletwa
na Yesu, matukio msingi kwa Wayahudi, Wakristo , na Waislamu. Aidha Papa kwa
mara ingine ametoa shukrani zake za dhati kwa Mwenye Heri Patriaki Fouad Twal ,
Maaskofu wa madhehebu mbalimbali, Mapadre, na Wafranciskani wenye kazi ya ulinzi
katika Maeneo Matakatifu. Shukrani zake pia amezitoa kwa Wakuu wa Nchi wa Jordan
, Israel na Palestina, kwa wema fadhila na mapokezi mazuri waliyompatia , yeye mwenyewe
pamoja na wale wote alioandamana nao katika ziara hii.
Baba Mtakatifu ametaja
malengo makuu ya ziara hii kuwa matatu, kwanza ni kwa ajili ya kuadhimisha miaka 50
ya mkutano wa kihistoria kati ya Papa Paulo VI na Patriaki Athenagoras . Hiyo ilikuwa
ni mara ya kwanza Mrithi wa Petro, kutembelea Nchi Takatifu . Ziara iliyo weka alama
msingi katika njia ya kutembea pamoja kuelekea umoja kamili wa Wakristu. Katika
ishara hii ya kinabii, Askofu wa Roma na Patriaki wa Constantinople kwa Pamoja,
walitolea sala zao katika kaburi la Yesu, wakiwa pia na Viongozi wengine wa Makanisa
mbalimbali na jamii, mamlaka ya kiraia na waamini wengi. Mahali hapo ambapo kunatoa
mwangwi mpya unao tangaza Ufufuko wa Kristo , waliweza kuyasikia upya uchungu wote
na mateso ya mgawanyiko kwamba bado upo kati ya wafuasi wa Kristo.Lakini juu ya yote
, katika mwitikio wa jibu linalo dai kuheshimiana kwa udugu na upendo, unaohimizwa
na sauti ya kubwa ya Mchungaji Mwema Mfufuka na peke , anayetaka wafuasi wake wawe
kundi mmoja . Na hivyo walipata hisia kali katika haja ya kuponya majeraha ambayo
bado yanaumiza na kuwa thabiti katika njia ya kuelekea ushirika kamili .
Papa
Francisko pia ametaja nia ya pili ya Hija yake , kwamba ilikuwa ni kuhimiza wale
wote wanaohusika na kazi ya kufanikisha amani kaika eneo la Mkoa wa Mashariki ya kati
na wale wote wanaotoa huduma za ubinadamu kwa watu wateswa hasa wakimbizi, watoto
, wazee na watu wengine dhaifu katika jamii, kutenda kwa bidii zaidi kufanikisha amani
na utulivu. Alikwenda kama Nabii wa Kitume, kuhimiza uwepo wa nyoyo za huruma,
kwa ajili ya watoto ya dunia hii ambayo kwa muda mrefu, imeishi na vita, wawe tena
na haki ya kukamilisha siku ya mwisho kwa amani ! Kwa nia hiyo, Papa ametoa wito
kwa Wakristo kuondoa uchungu kwakuwa moyo wazi na utulivu unao jazwa na Roho Mtakatifu,
kwa kuwa, uwezo wa ishara ya unyenyekevu , udugu na maridhiano, huweza kuhamisha
milima ya uchungu. Na hilo linawezekana kwa kuchukua tabia hiii ya unyenyekevu na
maridhiano katika maisha ya kila siku , kukubali kuishi na watu wa tamaduni na dini
mbalimbali , na hivyo kuwa mafundi wa amani. Papa alieleza kwa kukumbuka migogoro
ya Syria Israel na Palestina. Papa ametaja nia yake ya tatu kuhiji katika Nchi
Takatifu kwamba pia ilikuwa ni fursa ya kuthibitisha imani kwa jamii ya Kikristo,
ambao inakabiliwa na changamoto nyingi . Na pia kutoa shukrani za Kanisa zima kwa
uwepo wa Wakristo katika eneo hilo na katika Mashariki ya Kati . Hawa ndugu ni mashahidi
ujasiri wa matumaini na mapendo, " chumvi na mwanga" katika nchi hiyo. Kwa maisha
yao ya imani na sala , na kukubaliwa kwa shughuli za elimu na hisani, katika neema
ya maridhiano na msamaha , huchangia manufaa ya jamii.
Pamoja na Hija hii,
ambayo ilikuwa neema ya kweli ya Bwana, Papa alipenda kutoa neno la matumaini kwao
wote na kwake pia aliweza kupokea mengi kutoka ndugu zake wake kwa waume wenye kuwa
na matumaini, kwa njia ya mateso mengi , kama vile wale ambao walikimbia nchi yao
kwa sababu ya mapigano; kama wale wa wengi katika sehemu mbalimbali za dunia , ni
kudharauliwa na kubaguliwa kwa sababu ya imani yao katika Kristo. Sisi kuendelea kukaa
karibu nao ! Tunaomba kwa ajili yao na kwa amani katika Nchi Takatifu na katika Mashariki
ya Kati . Maombi ya Kanisa zima pia husaidia njia ya kuelekea umoja kamili miongoni
mwa Wakristo, ili ulimwengu upate kuamini katika upendo wa Mungu katika Yesu Kristo
amekuja kukaa miongoni mwetu.