2014-05-27 12:38:06

Useja ni zawadi ya neema kwa Mapadre toka wa Mungu


Papa anasema, useja ni zawadi ya neema kwa Mapadre toka kwa Mungu. Na si imani sadikifu ya Kanisa , na hivyo mlango ni wazi kwa mabadiliko, iwapo kanisa litapenda kufanya hivyo. .

Baba Mtakatifu Francisko, alieleza siku ya Jumatatu, wakati akijibu maswali ya wanahabari akiwa safarini kwa ndege, kurejea Roma , baada ya kukamilisha hija yake kwa mara ya kwanza katika Nchi Takatifu .Papa alionyesha imani yake kwamba, Padre Mkatoliki anapaswa kuishi maisha ya useja ingawa si sheria isiyoweza kubadilishwa na si moja ya kanuni katika mafundisho ya Kanisa.

Alisema Useja ni si “dogma, na hivyo Kanisa Katoliki halina kizuizi iwapo litapenda kuruhusu Mapdre kuoa kama wanavyo fanya makuhani katika baadhi ya Makanisa mengine ya Kikristo.

Useja ni kanuni ya maisha, anayochagua mtu wenyewe kw ahiarai yake, na yeye anaipenda zaidi na kuichukulia kama ni zawadi ya Mungu kwa Kanisa , na kwa kuwa siyo imani sadikifu ya Kanisa, mlango daima ni wazi katika mabadiliko . Kanisa hufundisha kwamba, Padre ni lazima akubali kwa moyo wote na kwa hiari kamili, kuitikia wito wa kujitolea bila ya kujibakiza kama mchumba wa Kanisa, kwa ajili ya utume wa Kanisa, kimsingi kuchukua Kanisa kama mke wake na kusaidia kutekeleza lengo lake.

Ingawa mapokeo ya utamaduni huu, yana historia ya karibia miaka 1,000, bado si sheria sadikifu ya kanisa, na uwepo wake hauhusiki imani ya kiroho au mafundisho ya Kanisa .Papa alieleza na kutaja kwamba, kumekuwa na shinikizo la kutaka kufanya mabadiliko na hasa kutokana na wingi kashfa ya unyanyasaji wa kijinsia zinazo fanywa na baadhi ya Mapadre na kulidhalilisha kanisa, na utetezi hiari wa useja katika Kanisa.

Kanisa limekuwa likijitetea kwamba, madhulumu ya ngono kwa watoto , iwe yanafanywa na Mapadre na watu wengine baki , ni tatizo la kijamii la watu wenye matatizo ya kisaikolojia.
Na kutokana na ukubwa wa tatizo , Kanisa haliwezi kuvumilia makosa yanayofanywa na watu wenye kasoro hiyo ya kisaikolojia. Na kwamba yeye mwenyewe ana mpango wa kukutana na wawakilishi wa kundi la waathirika wa unyanyasaji wa ngono mwezi ujao mjini Vatican. "Kanisa lina uvumilivu sufuri kwa kila kiongozi wa dini anayedhulumu mtoto kigono".
Mpango wa Papa kukutana na wawakilishi wa kundi la waathirika wa madhulumu ya ngono, baada ya Ibada ya Misa ambayo huongoza katika makazi yake mjini Vatican nyakati za asubuhi, kunaonyesha mshikamano wake mshikamano binafsi na kanisa kwa ujumla kwa watu hawa wanaoteswa na kitendo hicho cha aibu, kilichofanywa na Mapadre wabovu.







All the contents on this site are copyrighted ©.