Ujenzi wa amani,hudai zaidi ya yote, kuheshimu utu wa mtu na uhuru wa kila binadamu
Baba Mtakatifu Jumatatu akiwa katika Hija ya kutembelea maeneo Matakatifu Jerusalem
, pia alimtembelea Rais wa Israel, Mheshimiwa Rais Shimon Peres. Katika tukio hili,
Papa alipewa zawadi na watoto wawili na pia kuweka sahihi yake katika kitabu cha wageni
kilichopambwa kwa rangi ya dhahabu na kuwa na muda wa kubadilishana zawadi ukumbini
na kujadiliana hoja kadhaa mbele ya ujumbe kutoka pande zote mbili, Papa akiwa ameandamana
na Kardinali Pietro Parolin , Kardinali Sadri , Kardinali Tauran na Kardinali Kurt
Koch , pia Patriaki Twal na , Bruda Pizzaballa. Katika hotuba yake, Papa Francisko
, alimshukuru Rais Peres kwa mapokezi na ukarimu wake. Na kuonyesha furaha ya kukutana
nae tena mjini Jerusalem , mji wenye kutunza Maeneo Mtakatifu, mji mpendwa wa wafuasi
wa imani kuu tatu za kidini, wanao mwabudu Mungu mmoja aliyemwita Ibrahimu . Na kwamba,
maeneo Mtakatifu sio tu kuwa na makaburi au makumbusho kwa ajili ya watalii , lakini
mahali ambapo jumuiya za waamini kila siku hupata kielelezo cha imani na utamaduni
wao , na kutekeleza kazi yao ya upendo. Hasa kwa sababu hii , tabia yake ya utakatifu
ni lazima daima iimarishwe, kwa ajili ya urithi wa tangu kale si kwa manufaa ya
kizazi chetu tu lakini pia kwa vizazi vingine vijavyo. Inawezekana Yerusalemu kuwa
kweli mji wa amani !
Papa alisihi iwepo nia ya kudumisha utambulisho wake
na tabia yake takatifu ya kidini na utamaduni, kama jambo muhimu na kama hazina kwa
ajili ya watu wote! Na kwa jinsi gani mahujaji na wakazi wanavyoweza kufurahia kuzuru
Maeneo Mtakatifu bure na kwa hiari kushiriki katika sherehe za kidini.
Papa
aliendelea na hotuba yake akimtaja Mheshimiwa Rais Peres kuwa mtu anayejulikana kwa
fadhila zake za kuwa mtu wa amani na mpatanishi . Na alimstaajabia kwa mbinu ambazo
hujichukua kwa ajili ya kulinda amani, kwanza, kwa kudai heshima kwa utu wa mtu na
uhuru wa kila mtu , ambavyo Wayahudi, Wakristo na Waislamu wana imani sawa kwamba
kila binadamu ameumbwa na Mungu na wana matazamio ya uzima wa milele. Hii imani
ya kufanana, huwawezesha kujenga uthabiti wa kusimamia imara hoja hiyo , kuwa ndiyo
njia ya ufumbuzi wa amani katika kila hila na kila utata na migogoro. Na hapo alitoa
upya ombi lake kwa vyama vyote, kuepuka kila hila na kishawishi cha kutenda kinyume
namamuzi ya kuwa na amani, bali wakumbatie maamuzi yenye makubaliano ya kweli, kufanya
kazi bila kuchoka kwa ajili ya amani, mshikamano na umoja. Papa alisema, kuna
pia haja kwa Taasisi na vyama vya kijamii, kukataa yote yaliyo kinyume amani na
mahusiano ya kuheshimiana kati ya Wayahudi, Wakristo na Waislamu, na kujiepusha na
shari za kukimbilia vurugu na ugaidi, na kukataa kila aina ya ubaguzi kwa misingi
ya rangi au dini , na majaribio ya kulazimisha wengine imani za kidini, kwa gharama
ya haki za wengine, au dalili za kutovumilia kuelekezwa dhidi ya watu binafsi au maeneo
ya kuabudu, kwa kuwa wao ni Wayahudi au Wakristo au Waislamu. Papa alieleza
na kuomba kwamba, jamii ya Kikristo ya Israel iweze kuishi na kufanya kazi katika
Serikali ya Israeli, wakiwa kama sehemu ya jamii ya Israel wenye haki kamili ya
kushiriki kikamilifu katika mambo ya uraia , kisiasa na kiutamaduni. Wakristo wana
haki ya kuchangia na kushiriki katika utendaji wote kwa manufaa ya wote na ukuaji
wa amani ; wanataka kufanya hivyo kama raia kamili wenye nia ya kukuza maridhiano
na maelewano. Na alimthibitishia Rais Peres kwamba, humkumbuka katika sala na yeye
Rais na watu wa Israel kwa ujumla. Na pia anawaombea wote wale wanao kabiliwa na mateso
mbalimbali kwa sababu za ukatili wa kibinadamu. Amani iwe kwa taifa la Israel na Mashariki
yote ya Kati. Shalom! Kwa ajili ya kumbukumbu ya kukutana kwao, Papa Francisko
na Rais Shimon Peres, kwa pamoja walipanda mti wa mzeituni, katika bustani za Ikulu
Jerusalem.