Rais Giorgio Napolitano wa Italia amemwandikia Baba Mtakatifu Francisko ujumbe wa
matashi mema pamoja na kumkaribisha tena baada ya kuhitimisha hija yake ya kitume
Nchi Takatifu. Ni matumaini ya Rais Napolitano kwamba, hija na mwaliko uliotolewa
kwa Marais wa Israeli na Palestina wa kukutana na kusali pamoja na Papa Francisko
utakuwa ni kikolezo cha matumaini Ukanda wa Mashariki ya Kati, katika mchakato wa
kuendeleza majadiliano ya kutafuta haki na amani.
Ni hija ambayo imekoleza
majadiliano ya kidini na kiekumene kati ya Wayahudi na Waislam. Ni matumaini ya Rais
Giorgio Napolitano kwamba, mwaliko uliotolewa na Papa Francisko utagusa nyoyo za watu
wanaotamani kupata amani, maridhiano, upendo na mshikamano!