Mahakama kuu ya Malawi imesema kwamba, Rais Joyce Banda aliyekuwa anagombea nafasi
ya Urais kwenye uchaguzi mkuu uliopita hakuwa na mamlaka kikatiba ya kufuta uchaguzi
na kuitisha uchaguzi mwingine tena katika kipindi cha siku 90 kutokana na mapungufu
makubwa yaliyojitokeza katika mchakato wa uchaguzi huo!
Takwimu zinaonesha
kwamba, kuna idadi kubwa ya wapiga kura walioshiriki katika zoezi, ikilinganishwa
na namba halisi iliyokuwa kwenye Daftari la wapiga kura!
Viongozi wa kidini
nchini Malawi wanawataka wananchi kutulia na kudumisha amani na utulivu wakati huu
wakisubiri Tume Huru ya Uchaguzi Malawi kutangaza matokeo ya uchaguzi mkuu baada ya
kutokea itilafu kubwa wakati wa kupiga kura nchini humo!