Jumatatu Baba Mtakatifu Francisiko, aliifungua ratiba yake ya Hija katika nchi Takatifu
kwa kukutana na Mufti Mkuu wa Yerusalemu , katika Msikiti Mkuu wa Yerusalemu.
Na
katika nyayo za watangulizi wake, na hasa katika mwanga wa Paul VI , aliyefanya hija
hii miaka hamsini iliyopita, na hivyo kuwa Papa wa kwanza kutembelea Nchi Takatifu
,pia alitamani sana kufanya hija hii ya kutembelea maeneo ambayo yamemshuhudia Yesu
akiyaishi maisha haya ya kidunia. Na kwamba hija yake isingekuwa kamili bila ya kukutana
na kutafakari pamoja na watu wanao ishi katika nchi hii. Na hivyo kwa heshima na
taadhima ameweza kukutana na Mufti Mkuu wa Jerusalem , na Waislamu wengine , wake
kwa waume.
Hotuba ya Papa ilielekeza mawazo kwa Ibrahimu , ambaye aliishi
kama Mhujaji wa imani katika nchi hiI ambayo Waislamu, Wakristo na Wayahudi wanamtabua
Ibrahimu kuwa Baba yao wa Imani, ingawa kila mmoja, humwabudu Mungu Mmoja katika
njia tofaut. Ibarahim ni mfano mkubwa sana wa jinsi ya kumfuata Mungu kwa imani kuu.
Papa amewatia moyo waamini wote kwamba, katika Hija hii ya kidunia, hatuko
peke yetu. Kwa Wakristo, kwa njia ya msalaba, huungana na waamini wa dini nyingine
, kushiriki na kutembea pamoja na hata kuishi pamoja kama sehemu njia ya kutimiza
mapenzi ya Mungu. Papa alitoa shukurani zake za dhati kwa wote walio wezesha mkutano
huo na kwa ukarimu wao ulioonyesha kwamba , hija ya maisha, ni yetu sote binadamu
. . Papa aliomba uwepo wa mawasiliano ya kidugu na kubadilishana mawazo , kama
hatua yenye kutoa mwanya wa chaguzi na nguvu mpya, katika kukabiliana na changamoto
katika maisha ya kawaida, na wao kama viongozi waweze kuwa msitari wa mbele likabiliana
na changamoto kwanza.
Alisema, hawawezi kusahau ,ukweli kwamba Hija ya Ibrahimu,
pia ilikuwa ni wito kwa uadilifu : Mungu alimtaka aishuhudie imani yake kimatendo.
Na hivyo , pia wao, kama viongozi, wangependa kuwa mashahidi wa utendaji wa Mungu
katika dunia yetu. Aliomba kukutana kwao kutia shime vuguvugu la ndani la kusambaza
wito huu na katika kuwa mawakala wa amani na haki” . Papa aliwasihi katika zawadi
ya sala pia kujifunza kuwa na huruma kuu, kumheshimu kila mmoja na kupendana kama
kaka na dada ! Pia kujifunza kuelewa maumivu mwingine ! Na jina la Mungu lisitumiwe
kama chombo cha kuhalisha vurugu na maonevu, balijina hilo liwe kichocheo cha utendaji
wa pamoja kwa ajili ya kujenga haki na amani! Aidha Baba Mtakatifu , majira ya
asubuhi, alikutana na Rabbi Wakuu wawili wa Israel, na pia alitembelea Makao makuu
ya Rais wa Israel. Baba Mtakatifu majira ya jioni kabla ya kuongoza Ibada ya Misa
itakayokamilisha Hija yake katika nchi Takatifu , anakutana na Mapadre watawa na waseminaristi
katika Kanisa la Getsemani.