Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii,
anawaomba kumsindikiza kwa njia ya sala katika hija yake ya kitume huko Nchi Takatifu.
Baba Mtakatifu Jumamosi tarehe 24 anatembelea Amman nchini Yordan, Jumapili
tarehe 25 Mei 2014 atatembelea Palestina na kwa namna ya pekee mjini Bethelehemu na
Jumapili jioni, atakuwa Israeli na kilele cha hija hii ya kitume ni mjini Yerusalemu
atakapokutana na kusali pamoja na Patriaki Bartolomeo wa kwanza kama sehemu ya maadhimisho
ya Jubilee ya Miaka 50 tangu Papa Paulo VI alipokutana na Patriaki Anathegoras wa
Yerusalem.