2014-05-22 10:39:24

Watu wanalilia amani!


Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Barani Ulaya, CCEE, linawaalika waamini pamoja na watu wote wenye mapenzi mema kuungana na Baba Mtakatifu Francisko kwa sala wakati wa hija yake ya kitume Nchi Takatifu kwa ajili ya kuwaimarisha ndugu zake katika imani, matumaini na mapendo, kwa kuonesha ukaribu na mshikamano wa kidugu na wananchi wote huko Mashariki ya Kati.

Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Barani Ulaya linawapongeza Wakristo ambao licha ya hali ngumu wanayokabiliana nayo, lakini bado wameendelea kuwa ni mashahidi wa imani ya Kikristo. Hija ya Baba Mtakatifu Francisko ni hija ya kiekumene na Makanisa yote ya Kikristo, ili kwa pamoja yajielekeze zaidi katika mchakato wa ujenzi wa umoja na mshikamano wa Kanisa pamoja na kuendelea kulinda na kutunza maeneo matakatifu; mahali alipoteswa, kufa na kufufuka Kristo!

Ujumbe wa amani utakaotolewa na viongozi wa Makanisa uwe ni kikolezo kwa viongozi wa kisiasa huko Mashariki ya Kati kuongeza juhudi za kutafuta na kudumisha misingi ya haki, amani na utulivu, ili hatimaye, amani ya kudumu iweze kupatikana!







All the contents on this site are copyrighted ©.