2014-05-22 08:10:51

Watoto wanakabiliana na hali ngumu!


Watoto wanaoishi katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma iliyoko Kaskazini Mashariki wa Kenya wanakabiliana na mazingira hatarishi kwa usalama wa maisha na makuzi yao kwa sasa na kwa siku za usoni. Kuna watoto wanaokimbia vita na kinzani za kijamii kutoka kusini mwa Sudan na kuwasili kambini hapo pasi na usimamizi wa wazazi wala walezi wao. Kundi hili la watoto linahitaji huduma makini zaidi ili kukabiliana na mazingira magumu kwa sasa.

Taarifa ya Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa inaonesha kwamba, walau asilimia 71% ya wakimbizi wote duniani ni watoto wenye umri chini ya miaka 18. Idadi ya wakimbizi wanaofika kila siku inazidi kuongezeka kiasi kwamba, huduma msingi zinazotolewa kwa wakimbizi hawa zinasuasua.







All the contents on this site are copyrighted ©.