2014-05-22 10:04:54

Mafaniko ya uchumi ni lazima kuwiana na mipango ya elimu


Katika nyakati ambamo mna mwelekeo wa vijana wengi wa Afrika kuhamia mijini kuliko kubaki vijijini , ni muhimu kwa viongozi wa Afrika kuwa na mipango mizuri inayokidhi mahitaji ya makazi mapya ikiwemo , miundo mbinu na uzalishaji wa chakula kwa ajili ya kasi ya ongezeko la watu mijini, na pia kujali maendeleo na usalama wa wale wanaobaki vijijini . Ni makala ya Makhtar Diop, katika jarida la Benki ya Dunia, toleo la Mei 2014.

Amesema, pamoja na taarifa za uvumbuzi mpya wa mafuta, gesi na madini vinavyosikika kila mwezi , Afrika inahitaji kuwa na uwezo wa dondoo katika soko la dunia, na uwekezaji katika mapato mpya, hasa katika viwango vya juu vya elimu, afya , na vipaumbele vingine muhimu katika maendeleo endelevu.


Mwandishi ameeleza kwa kuangalisha katika ukweli kwamba, Afrika katika kipindi cha muongo mmoja uliopita imekuwa na mafanikio ya kipekee katika ukuaji wa uchumi,lakini bado Waafrika wengi wanaishi katika hali ngumu na umaskini wa kukithiri. Katika kipindi hicho uchumi ulikua katika kiwango cha wastani wa asilimia 4.5 kwa mwaka, kutoka na usimamizi makini katika uchumi . Na sasa, inakuwa ni muhimu kudumisha maendeleo hayo hasa katika kuwa na uchumi wenye kuwezesha kufuta umaskini wa kukithiri na kufanikisha elimu kwa watu wote wa bara la Afrika.

Na kwa kadri kunavyokuwa na msukumo mpya wa nguvu kwa watu kuhamia mijini, inalazimu pia kushughulikia kwa namna ya kipekee mahitaji mapya kwa ajili ya makazi , miundombinu, na uzalishaji wa kilimo kulisha wakazi wa mijini, na kuwa na uhakika wa chakula kwa maeneo ya vijijini pia.

Aidha ni muhimu kujali mabadiliko ya tabia nchi na mazingira , ambayo Afrika imeathiriwa kwa uwepo wa maafa kama ukame wa kukithiri, mafuriko na kupanda kwa viwango vya bahari ambavyo vimeleta a hasara za kiuchumi na ugumu wa maisha.

Wakati huo huo, changamoto hizi pia zichukuliwe kama fursa kwa ajili ya utafiti wa pamoja utakaowezesha wanasayansi duniani kote duniani kutenda kwa mshikamano na umoja kwa manufaa ya dunia nzima . Kwa namna hiyohiyo pia ni muhimu katika kuwa na ushirikiano sawia katika utafiti kati ya wanasayansi wa Afrika na nje ya nchi, hasa kwa ajili ya tiba, dawa, viumbe hai, kilimo cha umwagiliaji , uhandisi , madini na maeneo mengine.

Lakini mafanikio ya umoja katika utafiti inapaswa kuwa ni changamoto ya kusisimua barani iwapo kutafanyika masahihisho katika kosa la muda mrefu la kukosa usawa na uwiano katika mfumo wa elimu. Leo, hisa za wahitimu katika elimu ya juu bado zimelemea katika masomo ya sanaa na sayansi ya jamii, wakati sehemu ya wanafunzi katika sayansi, teknolojia, uhandisi, na hisabati , umebaki katika wastani wa chini ya asilimia 25. Na mbaya zaidi, kiwango kinashuka zaidi katika uwepo wa wanawake katika masomo ya sayansi na teknolojia.
Hata hivyo pamoja na hayo, shukrani kwa maendeleo ya hivi karibuni ya elimu kwa wote , juhudi zilizofanikisha watoto wengi kuandikishwa katika mfumo wa elimu ya msingi barani Afrika, zaidi na zaidi ya wanafunzi wanakamilisha elimu ya msingi na sekondari . Juhudi hizi zinaleta matumaini kwamba, kizazi kipya cha vijana Waafrika, kitakuwa na elimu na ujuzi wa kisasa na maarifa yanayohitajika kupata ufumbuzi dhidi ya changamoto ya Afrika.








All the contents on this site are copyrighted ©.