Mfalme wa Bahrein akutana na kuzungumza na Papa mjini Vatican
Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu tarehe 19 Mei 2014 amekutana na kuzungumza na Mfalme
Hamad Bin Isa Al Khalifa wa Bahrein ambaye baadaye alibahatika kuzungumza na Kardinali
Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican aliyekuwa ameambatana na Askofu mkuu Dominique
Mamberti, Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.
Viongozi
hawa wamejadiliana masuala muhimu katika maisha ya mwanadamu kwa kujikita zaidi katika
mchakato wa amani na utulivu huko Mashariki ya Kati pamoja na kukazia majadiliano
yatakayoihusisha Jamii.
Kwa pamoja wamepongeza mchango unaotolewa na Wakristo
huko Bahrein, lakini kwa namna ya pekee kabisa Kanisa Katoliki katika huduma kwa wananchi.