2014-05-19 09:06:29

Jumuiya ya Kimataifa inashutumu adhabu ya kifo kwa Meriam kutoka Sudan


Hukumu ya adhabu ya kifo iliyotolewa kwa Meriam Yahya Ibrahim Ishaq kutoka Sudan kwa kuolewa na Mkristo raia wa Sudan ya Kusini, inaendelea kupingwa katika majukwaa ya kimataifa, kiasi kwamba, habari hizi zimemfikia Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki-Moon. Wakili wa Mama huyu amekata rufaa na kwa sasa wanasubiri uamuzi kutoka kwa Mahakama kuu ya Rufaa kutoa majibu.

Mama huyu ambaye amezaa mtoto mmoja na ana mimba kwa sasa anasema tangu awali amekuwa ni Mkristo na wala hajawahi hata siku moja kuwa mwamini wa dini ya Kiislam. Wakati huo huo, Serikali ya Sudan inasema kwamba, ina dhamana ya kusimamia haki msingi za binadamu na uhuru wa kidini kadiri ya Katiba ya nchi ya Mwaka 2005 pamoja na sheria za nchi.

Ufafanuzi huu umetolewa na Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Sudan baada ya kupata shinikizo kutoka katika Jumuiya ya Kimataifa kuhusu uvunjwaji wa haki msingi za binadamu na uhuru wa kuabudu!







All the contents on this site are copyrighted ©.