2014-05-19 07:59:14

Changamoto katika ujenzi wa misingi ya haki, amani na upatanisho!


Patriaki Beshara Rai wa Kanisa la Wamaronite kutoka Lebanon anatarajiwa kushiriki katika hija ya kichungaji itakayofanywa na Baba Mtakatifu Francisko katika Nchi Takatifu kuanzia tarehe 24 hadi tarehe 26, Mei 2014 na inayoongozwa na kauli mbiu, ili wote wawe wamoja! RealAudioMP3

Taarifa zinaonesha kwamba, hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa kiongozi wa dini kutoka Lebanon kutembelea Yerusalemu, tangu mwaka 1948. Hii ni changamoto ya ujenzi wa misingi ya haki, amani na upatanisho kati ya mataifa, kwa kukazia mafao ya wengi, uhuru na mshikamano wa kimataifa katika kukabiliana na changamoto za maisha ya watu.

Itakumbukwa kwamba, Lebanon na Israeli ni nchi ambazo bado zinaangaliana kwa “macho ya makengeza” kiasi kwamba, wananchi wa Lebanon hawaruhusiwi kutembelea eneo la Israeli. Kadiri ya sheria za Israeli, viongozi wa Kanisa wanaruhusiwa kutembelea Israeli ili kutoa huduma kwa waamini wapatao 10, 000 wa Kanisa la Maronite.

Patriaki Beshara Rai anasema, hija ya kiekumene itakayomwezesha kukutana na Baba Mtakatifu Francisko pamoja na viongozi wengine wa Makanisa ni hija ya kidini na wala haina uhusiano wowote na masuala ya kisiasa.








All the contents on this site are copyrighted ©.