Askofu mkuu mteule Damian Dennis Dallu wa Jimbo kuu la Songea, Tanzania aliyeteuliwa
hivi karibuni na Baba Mtakatifu Francisko anatarajiwa kusimikwa rasmi kama kiongozi
mkuu wa Jimbo kuu la Songea, Jumapili tarehe 18 Mei 2014.
Akizungumza
na Radio Vatican, Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki
Tanzania na aliyekuwa msimamizi wa kitume wa Jimbo kuu la Songea anasema, Familia
ya Mungu Jimbo kuu la Songea, imejipanga vyema kumkaribisha Askofu mkuu Dallu ambaye
hadi uteuzi wake alikuwa ni Askofu wa Jimbo la Geita.
Rais wa Baraza la Maaskofu
Katoliki Tanzania anaiomba Familia ya Mungu Jimbo kuu la Songea kumpokea Askofu mkuu
Dallu kwa mikono miwili na kumpatia ushirikiano wa dhati, ili kwa pamoja waweze kushikamana
kulijenga na kuliendeleza Jimbo kuu la Songea kadiri ya mapenzi Mungu.