Papa kutembelea Madhabahu ya "Divino Amore" wakati mwingine, lakini si Jumapili ijayo!
Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican anasema kwamba, Baba Mtakatifu Francisko
ameahirisha ziara yake ya kutembelea kwenye Madhabahu ya Bikira Maria wa "Divino Amore"
yaliyoko mjini Roma hadi hapo itakapotangazwa tena.
Baba Mtakatifu alikuwa
anatarajiwa jumapili ijayo kutembelea na kusali kwenye Madhabahu ya "Divino Amore"
nyakati za jioni, lakini kwa sasa ziara hii imefutwa ili kumpatia nafasi Baba Mtakatifu
kujiandaa zaidi kwa ajili ya hija yake ya kichungaji, anayotarajia kuifanya huko Nchi
Takatifu kuanzia tarehe 24 hadi tarehe 26 Mei 2014, ikiongozwa na kauli mbiu, wote
wawe wamoja!