2014-05-15 12:21:39

Apewa adhabu ya kifo kwa kuolewa na Mkristo!


Mahakama moja nchini Sudan imemkuta na hatia Meriam Yahya Ibrahim Ishaq, mwanamke mwenye umri wa miaka 27 ya kukufuru na kuzini kwa kuwa ameolewa na raia mmoja Mkristo kutoka Sudan ya Kusini na hivyo kuhukumiwa kuchapwa viboko mia moja na kunyongwa hadi kufa!

Adhabu hii imewashtua watetezi wa haki msingi za binadamu, kwa kuitaka Serikali ya Sudan kuheshimu uhuru wa kuabudu kadiri ya Katiba ya nchi iliyotungwa kunako Mwaka 2005.

Mahakama hiyo imetumia "Sharia" za dini ya Kiislam zilizoingizwa nchini humo kunako mwaka 1983 zinazopiga rufuku kwa mwamini wa dini ya Kiislam kuoa au kuolewa na Mkristo. Viongozi mbali mbali wa Jumuiya ya Kimataifa wameitaka Serikali ya Sudan kuingilia kati ili kusitisha utekelezaji wa adhabu hii ambayo ni kinyume cha haki msingi za binadamu.







All the contents on this site are copyrighted ©.