Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya Katekesi yake siku ya Jumatano, tarehe 14 Mei
2014 amesali kwa namna ya pekee kwa ajili ya kuwaombea wachimba mgodi huko Soma, nchini
Uturuki, waliofariki dunia baada ya kufunikwa na kifusi na bado kuna kundi kubwa la
wachimba mgodi ambalo bado halijukilani liliko. Baba Mtakatifu anawaombea wote waliofariki
dunia pamoja na familia zao, ili waweze kupata faraja kutoka kwa Mwenyezi Mungu, mwingi
wa huruma na mapendo.
Baba Mtakatifu Francisko pia amewakumbuka wahamiaji na
wakimbizi waliofariki maji kwenye Bahari ya Mediterania, wakati wakijaribu kuvuka
kutoka Afrika kwenda Ulaya. Baba Mtakatifu anasema, haki msingi za binadamu zinapaswa
kupewa kipaumbele cha kwanza pamoja na Jumuiya ya Kimataifa kuunganisha nguvu zake
kwa ajili ya kuokoa maisha ya watu wanaofariki dunia huko Baharini.