Familia ya Mungu Jimbo kuu la Venezia inatangaza kifo cha Kardinali Marco Cè, Patriaki
mstaafu wa Jimbo kuu la Venezia kilichotokea, tarehe 12 Mei 2014 kwenye Hospitali
ya Watakatifu Yohane na Paulo mjini Venezia, alikokuwa amelazwa tangu tarehe 19 Machi
2014 baada ya kuvunjika mguu. Tarehe 13 Aprili 2014 akapewa Sakramenti ya Mpako wa
Wagonjwa.
Kardinali Cè alizaliwa tarehe 8 Julai 1925 Jimboni Cremona. Baada
ya masomo na majiundo yake ya kikasisi, akapadrishwa kunako tarehe 27 Machi 1948.
Tarehe 22 Aprili 1970 akateuliwa na Mtumishi wa Mungu Papa Paulo VI kuwa Askofu msaidizi
wa Jimbo kuu la Bologna. Tarehe 7 Desemba 1978 akateuliwa na Mtakatifu Yohane Paulo
II kuwa Patriaki wa Venezia.
Tarehe 30 Juni 1979 akateuliwa kuwa Kardinali
wa Venezia ambako amewatumikia Watu wa Mungu kwa kipindi cha miaka 23 na kung'atuka
kutoka madarakani hapo tarehe 5 Januari 2002.