2014-05-11 12:23:01

Usimamizi wa maliasili uwausishe zaidi wananchi!


Kiongozi wa UNDP aliyeko ziarani nchini Tanzania, Helen Clark, amesema usimamizi wa maliasili unaoshirikisha jamii ni ufumbuzi wa muda mrefu na wenye ufanisi zaidi kwa ya kudhibiti vitendo vya ujangili wa tembo na biashara haramu ya wanyamapori. Akizungumza Jumapili tarehe 11 Mei 2014 na watu kutoka vijiji 21 karibu na Hifadhi ya Taifa Ruaha alijifunza uzoefu wao na changamoto za usimamizi katika uhifadhi wa wanyamapori.

'Ni wazi,' alisema, 'kila mtu katika jamii, ikiwa ni pamoja na wanawake, vijana na wazee, wana wajibu katika uendelezaji wa ulinzi wa wanyamapori na jamii karibu na maeneo ya hifadhi. Mipango ya jamii lazima ipewe msaada inayostahili ili kuzalisha mapato kwa ajili ya watu wa vijijini na kusaidia kuleta njia mbalimbali za mapato kupitia utalii na sekta nyingine za huduma, 'alisema.

Helen Clark alitembelea Hifadhi ya Taifa Ruaha, Iringa, mkoa uliopo kusini mwa Tanzania kuangalia matokeo ya mradi wa uhifadhi wa UNDP na Mfuko wa Dunia wa Mazingira uliolenga uhifadhi wa wanyamapori na mazingira ya Kusini mwa mzunguko wa Tanzania, ikiwa ni pamoja na maeneo ya hifadhi ya Ruaha, Kitulo, Mpanga Kipengere na Mlima Rungwe.

Kupitia msaada wa UNDP wa kiufundi na fedha, mradi ulifanya sensa ambayo ilionesha kupungua kwa dhahiri kwa idadi ya tembo katika mfumo wa ikolojia wa Ruaha-Rungwa, ikiwa ni upungufu kutoka tembo 31,625 mwaka 2009 hadi 20,090 tu mwaka 2013. Kwa hiyo mradi ulianzisha shughuli za kuisaidia Wizara ya Maliasili na Utalii katika maendeleo ya mkakati wa taifa wa kupambana na biashara ya wanyamapori.

Msaada wa UNDP uliwezesha ununuzi wa matingatinga. Uongozi wa Hifadhi umeanza uboreshaji wa barabara ambao utafungua eneo hilo kwa ajili ya kuongeza fursa za utalii, usalama bora zaidi, na vilevile kuwezesha doria ya mara kwa mara kwa ajili ya kupambana na ujangili.

Sehemu kubwa ya kazi hii imekuwa kuimarisha utawala katika taasisi za kitaifa zinazohusika na usimamizi wa wanyamapori na utekelezaji; kuimarisha maisha ya jamii na mipango ya kugawana faida ili kupunguza kichocheo kwa jamii hizo kuajiriwa katika shughuli za ujangili unaofanywa na magenge ya wahalifu.








All the contents on this site are copyrighted ©.