Papa anawaombea wasichana waliotekwa nyara Nigeria
Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anapenda
kuungana na wananchi wa Nigeria pamoja na Jumuiya ya Kimataifa kusali kwa ajili ya
kuachiliwa kwa wasichana mia mbili waliotekwa nyara na Kikundi cha Boko Haram nchini
Nigeria hivi karibuni.
Hii ni kampeni ya kimataifa ambayo inawahusisha viongozi
mbali mbali na watu maarufu, ili kushinikiza Kikundi cha Boko Haram kuwaachilia huru
wasichana waliotekwa, ili waweze kujiunga na familia zao na hatimaye kuendelea na
masomo yao!