2014-05-10 10:41:13

Ufaransa kula sahani moja na vikundi vya kigaidi Afrika!


Waziri wa ulinzi wa Ufaransa Jean Ives Le Drain anasema kwamba, Ufaransa itapeleke kikosi cha wanajeshi elfu tatu, Kaskazini mwa Afrika ili kupambana barabara na vikundi vya kigaidi ambavyo vimeendelea kusababisha maafa makubwa kwa wananchi wa Afrika ya Kaskazini.

Kikosi cha askari elfu moja, kitaendelea kubaki nchini Mali, ili kuhakikisha ulinzi na usalama wa wananchi na mali zao. Itakumbukwa kwamba, wanajeshi kutoka Ufaransa wako nchini Mali tangu Januari 2013 baada ya Umoja wa Mataifa kuomba Ufaransa kusaidia juhudi za kudumisha amani nchini Mali na katika nchi jirani.







All the contents on this site are copyrighted ©.