Baraza la Kipapa la Familia kwa kushirikiana na Shirika la Misaada la Kanisa Katoliki
Italia, Caritas linaendelea kuhamasisha upatikanaji wa amani kwa ajili ya familia
za wananchi wa Syria, kwa kuwataka wahusika wakuu kujikita katika majadiliano ili
kumaliza vita hii ambayo imeendelea kusababisha maafa makubwa kwa wananchi wasiokuwa
na hatia.
Wanataka pia watu wote waliotekwa nyara kuachiliwa huru. Caritas
Italia itaendelea kutoa msaada wake wa hali na mali kwa wanachi wa Syria katika kipindi
hiki kigumu pamoja na kusaidia jitihada za kuwafunda watu umuhimu wa amani na mshikamano
wa dhati.
Baraza la Kipapa la Familia pamoja na Caritas, Italia linatoa ujumbe
huu ambao uko kwenye mfumo wa video kwenye Maonesho ya Vitabu yanayofanyika kuanzia
tarehe 8 hadi tarehe 12 Mei, 2014 huko mjini Torino, Kaskazini mwa Italia. Vatican
inashiriki pia katika maonesho ya vitabu huko Torino kama mjumbe wa heshima.