Ni ruksa kutembelea Ikulu ndogo ya Castel Gandolfo
Baba Mtakatifu Francisko hivi karibuni ameridhia wazo la kufungua milango kwa Jamii
kutembelea Ikulu Ndogo ya Castel Gandolfo na viunga vyake, iliyojengwa kunako tarehe
10 Mei 1626 wakati Papa Urbano wa VIII alipoanza kutumia Ikulu ndogo ya Castel Gandolfo
kama makazi ya Kipapa wakati wa kiangazi. Haya ni makazi ambayo yamekuwa pia ni kimbilio
la watu wengi wakati wa vita kuu ya pili ya dunia, Papa Pio wa XII alipotoa hifadhi
kwa wakimbizi waliokuwa wanatafuta njia ya kuhifadhi maisha yao.
Hivi ndivyo
anavyosimulia Dr Osvaldo Gianol aliyeteuliwa hivi karibuni kuwa ni Msimamizi mkuu
wa Ikulu Ndogo ya Castel Gandolfo, kwa kutoa mwaliko kwa watalii wa ndani na nje ya
Italia kutembelea Ikulu Ndogo ya Castel Gandolfo ili kujionea wenyewe maajabu ya Mungu
kwa njia ya mikono ya wanadamu. Watalii watapata fursa ya kutembelea pia Bustani zilizoko
Castel Gandolfo pamoja na kupata maelezo ya kina yanayogusa historia na umuhimu wake.
Akizungumzia
kuhusu jitihada hizi, Dr Antonio Paolucci, Mkurugenzi wa Makumbusho ya Vatican anasema,
ndani ya Bustani ya Ikulu Ndogo ya Castel Gandolfo, watalii wataweza kuona mambo mengi
ya kihistoria, sehemu ya mapumziko na mahali pa kuvulia samaki, kwani Ikulu Ndogo
ya Castel Gandolfo imejengwa kwenye ukingo wa Ziwa. Samaki wanaovuliwa ziwani humo
wakati wa majira ya kiangazi ni kwa jili ya kusaidia watu wenye shida mbali mbali.
Matembezi
kwenye Bustani za Ikulu Ndogo ya Castel Gandolfo yanaweza kufanyika kwa muda wa saa
nzima na yataendelea kusimamiwa na Mkurugenzi wa Makumbusho ya Vatican, ambaye bado
“anakuna kichwa” ili kuweka bayana mikakati iitakayowawezesha watalii kufaidika na
matembezi watakayofanya ndani ya Ikulu Ndogo ya Castel Gandolfo. Matembezi haya yamefunguliwa
rasmi hapo tarehe Mosi Machi 2014.
Kwa sasa watalii hawataweza kutembelea ndani
ya vyumba vya Ikulu Ndogo ya Castel Gandolfo kwani hii ni ziara inayohitaji mikakati
makini ya ulinzi na usalama. Matokeo ya sasa yatasaidia kuweka mikakati kwa siku za
usoni. Wafanyakazi wa Ikulu Ndogo ya Castel Gandolfo wamepokea wazo hii kwa furaha
kwani ni fursa itakayowawezesha kutumia weledi wao kwa mapana zaidi.
Wananchi
wa Castel Gandolfo wanafurahia kwa sababu mbali mbali hasa zaidi kwa kukuza na kuendeleza
utalii katika eneo hili. Uongozi wa Makumbusho ya Vatican unawahimiza watalii kufanya
ziara za makundi ili kupata watu watakaowaongoza na kuwaelekeza.