Katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, Baba Mtakatifu Francisko anawaomba
viongozi wa kisiasa kuzingatia mambo makuu mawili: utu na heshima ya binadamu na mafao
ya wengi. Wafanyakazi sehemu mbali mbali duniani wameiadhimisha siku hii kwa maandamano
makubwa, semina na mikutano maalum pamoja na kutoa zawadi kwa wafanyakazi bora. Wale
waliosahaulika kwa mwaka huu, wasikate tamaa, waendelee kuongeza juhudi, bidii na
maarifa katika kazi.