Walioguswa na miujiza ya Mtakatifu Yohane Paulo II
Mama Floribeth Mora Diaz, aliyepata bahati na neema ya kupona kutokana na ugonjwa
wake kwa maombezi ya Mtakatifu Yohane Paulo II, ndiye aliyeteuliwa kubeba Masalia
ya Mtakatifu Yohane Paulo II wakati wa Ibada ya Misa Takatifu, kwenye Uwanja wa Kanisa
kuu la Mtakatifu Petro mjini Vaticam siku ya Jumapili tarehe 27 Aprili 2014.
Masalia
ya Mtakatifu Yohane XXIII yamebebwa na wapwa zake wanne, waliokuwa wameongozana na
Meya wa Mji wa Sotto Il Monte, Mstahiki Eugenio Bolognini ambaye pia ni Rais wa Mfuko
wa Yohane XXIII. Sr. Marie Simon-Pierre, aliyeponywa kutokana na maombezi ya Mtakatifu
Yohane Paulo II amesoma ombi kwa lugha ya Kifaransa katika Ibada hii.