2014-04-25 15:48:53

Vatican iko tayari kwa Maadhimisho!


Padre Federico Lombardi, Msemaji mkuu wa Vatican anasema maandalizi ya maadhimisho ya kutangazwa kwa Wenyeheri Yohane XXIII na Yohane Paulo II kuwa watakatifu yataanza kutimua vumbi siku ya Jumamosi, mikesha itakayofanywa kwenye Makanisa mbali mbali mjini Roma, kielelezo cha mshikamano wa maisha ya kiroho. Ibada katika Makanisa zitaendeshwa katika lugha mbali mbali.

Ibada ya Misa takatifu inatarajiwa kuhudhuriwa na Viongozi na wawakilishi wa dini na madhehebu mbali mbali ya Kikristo, kuna wajumbe 93 wanaowakilisha nchi 24 na kati yao kuna viongozi wakuu wa Serikali, Malikia na Wafalme. Makardinali 150, Maaskofu 1000. Kuna Mapadre 870 watakaoshiriki kugawa Ekaristi Takatifu

Jumapili asubuhi, Ibada itaanza kwa Rozari ya Huruma ya Mungu, hapo saa 3:00 asubuhi, ikisindikizwa na nyimbo kutoka katika kwaya mbali mbali za Roma, Bergamo na Poland.









All the contents on this site are copyrighted ©.