Waziri mkuu wa Albania Bwana Edi Rama akutana na kuzungumza na Papa Francisko mjini
Vatican
Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi tarehe 24 Aprili 2014 amekutana na kuzungumza na
Waziri mkuu wa Albania Bwana Edi Rama, ambaye baadaye amekutana pia na Kardinali Pietro
Parolin, Katibu mkuu wa Vatican aliyekuwa ameambatana na Askofu mkuu Dominique Mamberti,
Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.
Viongozi
hawa wawili wamezungumzia kuhusu uhusiano kati ya pande hizi mbili, lakini zaidi wakajikita
katika tema zinazogusia masuala ya kimataifa, kikanisa na kiraia: Wameangalia kwa
pamoja umuhimu wa majadiliano ya kidini na mchango wa Kanisa katika ustawi na mafao
ya wengi nchini Albania. Wamegusia pia masuala ya kikanda na safari inayotekelezwa
na Albania ili kuweza kujiunga na Umoja wa Ulaya.