Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anatamka
kwamba, Kristo amefufuka, Alleluiya. Baba Mtakatifu anaendelea kusema kwamba, kila
mara mwamini anapokutana na Kristo anakirimiwa furaha ya kweli inayopata chimbuko
lake kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Kwa maneno haya ya Baba Mtakatifu Francisko,
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican inakutakia kheri na baraka katika Maadhimisho
ya Siku kuu ya Pasaka kwa Mwaka 2014.