2014-04-20 17:08:15

Ujumbe wa Papa wa Pasaka wawakumbuka wanaoteseka kwa njaa, vita na uonevu.


Baba Mtakatifu Francisko, katika Jumapili ya kwanza ya Pasaka, ya Huruma Takatifu, mapema aliongoza Ibada ya Misa, katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro. Ibada ilihudhuriwa na umati wa watu zaidi ya 150,000. Baada ya Ibada hiyo majira ya adhuhuri kama kawaida ya siku hii kwa Mapapa, kutokea dirisha lake la kujisomea, alitoa ujumbe na baraka zake za Pasaka kwa Jiji la Roma na Dunia kwa Ujumla, Urbi et Orbi ..
Katika ujumbe huo amesema, Ndugu zangu wapendwa, Heri ya Siku Kuu Takatifu ya Pasaka! Kanisa duniani kote, limetafakari maneno ya Malaika kwa wanawake. Msiogope, Nafahamu mnamtafuta Yesu aliyesulubiwa. Hayuko hapa. Maana amefufuka. Njoni, muone mahali alipokuwa amelazwa "(Mt 28:5-6 ). Msiwe na woga wala hofu! Bwana Mfufuka !

Papa amefafanua kwamba, hiki ndicho kilele cha tangazo la Injili, Ni habari Njema, : Yesu, ambaye alisulubiwa, amefufuka ! Tukio hili ni msingi wa imani ya Mkristo na tumaini lake. Kama Kristo asinge fufuka , Ukristo ulikuwa umepoteza maana yake ; ujumbe na utume wote wa kanisa ungekuwa ni bure , kwa kuwa, Ufufuko wa Kristo, ndiyo jambo msingi la kwanza katika Utume wote ya Kanisa tangu mwanzo wake kuendelea milele yote, kwamba Kristo amekishinda kifo na kutuletea uzima wa milele. Huo ndiyo ujumbe, Wakristo wanaoutoa kwa dunia leo hii: Yesu , Upendo wa Mungu uliomwilishwa, na aliye sulubiwa Msalabani , kwa ajili ya dhambi zetu, lakini Mungu Baba Yake na Bwana wa maisha na kifo, alimfufua. Kwa jina la Yesu , Upendo ameshinda juu ya chuki, huruma juu ya dhambi, wema juu ya maovu , ukweli juu ya uwongo, maisha juu ya kifo.

Na hiyo ndiyo maana Wakristo huwaambia watu wote, “Njoo nyote na muone, watu wa kila hali ya maisha ya binadamu ,wanaojiweza, wadhaifu na wanyonge, wenye dhambi na mlio walio katika hali ya kifo , Habari Njema ni kwenu nyote! NI maneno ya ushahidi wa ushindi mwaminifu wa upendo, unaotutaka kuondoka katika maisha ya kale na kukutana na watu wengine, kuwa karibu na wale wanao angamizwa kwa matatizo ya maisha , kushirikiana na masikini , wale walio simama kando ya upande wa wagonjwa, wazee n.k " Njoo! uone Upendo wenye nguvu zaidi , Upendo wenye kutoa uzima wa milele, upendo wa matumaini ya maua katika jangwa.


Kwa hakika hii furaha katika mioyo yetu, na leo hii pia wewe tunakuambia, Bwana kufufuka. Baba Mtakatifu baada ya maelezo hayo , alitoa wito kwa watu wote, waliwezeshe Kanisa kuwafikia na kuwapa habari kwamba kuna Baba wala si yatima, kwamba Kanisa linawapenda kuwaalika kuabudu pamoja nawe.

Papa pia ametoa wito kwa wahusika wote , watoe msaada wa kushinda janga la njaa , hasa linachochewa na uwepo wa migogoro na matumizi mabaya ambayo mara nyingi ni binadamu kukosa kuwajibika.
Kuliwezesha Kanisa kulinda mazingira magumu , hasa watoto, wanawake na wazee, kama matokeo ya dhuluma unyanyasaji na kutelekezwa. Pia kuliwezesha Kanisa kutoa huduma kwa ndugu na dada zetu waliopigwa na mlipuko wa ugonjwa Ebola katika Guinea Conakry, Sierra Leone na Liberia, na pia kutoa huduma kwa wanaosumbuliwa magonjwa mengine mengi ambayo pia huenezwa kwa sababu ya kutelekezwa na umaskini.

Pia Papa ameomba Faraja kwa wale ambao hawawezi kusherehekea hii Pasaka na wapendwa wao kwa sababu ya ukosefu wa haki , haki yao imechanwa, na upendo wao kunyakuliwa , kama ilivyo kwa watu wengi , wakiwa ni makuhani na waamini, walio sehemu mbalimbali za dunia, ambao wametekwa nyara, na wakimbizi pia, watu waliolazimika kuhama makazi yao ya kudumu na sasa wanaishi katika hali duni za kusikitisha, ubinadamu wao ukifinyangwa finyagwa na kukosa hata uhuru wa kukiri imani yao kwa uhuru.


Tunakuomba , Bwana Yesu, ukomeshe vita, kila migogoro, iwe mikubwa au ndogo, ya kale au ya hivi karibuni.

Na kwa namna ya pekee papa aliitaja taifa pendwa la Syria linalopita katika wote mateso na madhara ya mgogoro wa kisiasa, ili watu wa eneo hilo wasiokuwa na hatia waweze kupokea msaada wa kibinadamu na kwamba, kusitisha utumiaji wa nguvu mauti , hasa dhidi ya watu wasio weza kujitetea wenyewe , badala yake wajawe na ujasiri wa kujadili amani ya muda mrefu, muafaka wa muda mrefu unao subiriwa. Papa pia aliitaja migawanyiko na vurugu katika taifa la Iraki, Israel na Palestina.

Pia aliligeukia bara ya la Afrika na kuomba kwa ajili ya kufikishwa mwisho migogoro katika Jamhuri ya Afrika ya Kati na mashambulizi ya kikatili ya kigaidi katika maeneo ya Nigeria na vitendo vya unyanyasaji katika Sudan ya Kusini.

Na pia uwepo wa nyoyo za maridhiano na kindugu katika taifa la Venezuela.

Kwa ufufuko Bwana , ambamo mwaka huu Wakristu wa makanisa yote wamesherehekea Siku Kuu hii pamoja na wale wanao fuata kalenda ya Juliana, Bwana na aangazie nakuvuvia juhudi za kukuza amani Ukraina ili kwamba wale wote wanaohusika katika jumuiya ya kimataifa waweze kufanikisha juhudi za kuzuiia ghasia , katika roho ya umoja na mazungumzo, na kuonesha njia kwa ajili ya baadaye ya nchi , kama ndugu na kwamba wote waweze kupaza sauti zao na kusema, Christos Voskrese !" [ Kristo Kafufuka !]









All the contents on this site are copyrighted ©.