2014-04-20 11:58:07

Turudi Galilaya kuigundua upya Neema ya Mungu- Papa


Baba Mtakatifu Francisko, amehimiza waamini kutafakari upya maana ya wito wao katika ubatizo , alikokuita “kurudi Galilaya”, kuyasoma upya maisha ya Yesu katika misingi ya msalaba na ushindi wake, kwa tendo kuu la upendo. Papa alieleza katika homilia yake, wakati akiongoza Maadhimisho ya Mkesha wa Pasaka katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, mjini Vatican .
Ametoa wito kwa kila Mkristu kugundua upya neema za ubatizo wao kama chemichemi ya maisha , yanayochota nguvu kutoka vyanzo vya imani na uzoefu wa maisha ya Kikristo. Kurudi Galilaya inamaanisha ni kurudi zaidi ya yote katika mwanga ule ambamo mna neema ya Mungu iliyougusa moyo tangu mwanzo wa kujiunga katika hija ya maisha ya Kikristo.
Papa alieleza kuwa, Injili ya ufufuo wa Yesu Kristo huanza na safari ya wanawake kaburini alfajiri siku baada ya Sabato. Wao walikwenda kaburini, kwa ajili ya kutoa heshima zao kwa mwili wa Bwana , lakini waliona kaburi li wazi na tupu . Malaika mmoja mwenye nguvu akawaambia : "Msiongope ninyi, kwa maana najua kuwa mnamtafuta Yesu aliyesulubiwa. Hayupo kwani amefufuka kama alivyosema..... (Mt 28:5) nendeni mkawaambie wanafunzi wake, amewatangulia Galilaya " (V. 7) . Wanawake haraka waliondoka na njiani walikutana na Yesu aliyewaambia msiogope ; nendeni mkawaambie ndugu zangu waende Galilaya ; wao huko wataniona "(mstari 10).

Baada ya kifo cha Mwalimu wao, wanafunzi wa Yesu walitawanyika ; imani yao alikuwa imeshuka, kila jambo lilioonekana kama kufikia ukomo wake, walikosa uhakika na matumaini yao kuwa kama yamekufa. Lakini sasa, ujumbe wa wanawake wa kushangaza kama ilivyokuwa, uliwafikia kama mwali wa mwanga mkali katika giza nene. Habari ya Yesu kufufuka ilienea kama alivyosema. Na hata ile habari ya kwenda Galilaya waliyokuwa wameisikia wanawake mara mbili, kwanza kutoka kwa malaika na kisha kutoka kwa Yesu mwenyewe: Waende Galilaya ;huko watamwona, inawachoma moyo. .

Papa alikumbusha Galilaya palikuwa ni mahali wanafunzi walipoitwa kwa mara ya kwanza. Na sasa ni kurudi huko, mahali ambako waliitwa mara ya kwanza, ambako Yesu akitembea katika mwambao wa ziwa , aliwaona wavuvi wakitwika nyavu zao , na kuwaita na waliacha nyavu zao , wakamfuata (cf. Mt 4:18-22) .

Papa anafafanua kwamba , kurudi Galilaya maana ya kutafakari upya yote, kwa misingi ya msalaba na ushindi wake . Tena ni kusoma kila kitu - mahubiri ya Yesu , miujiza yake, jamii mpya , msisimko na usaliti huu, hata usaliti mpya, ni kusoma kila kitu kuanzia mwanzo hadi mwisho , matendo yote ya upendo wa Yesu, hadi tendo hili kuu la upendo .

Pia kwa kila mmoja wetu, kuna Galilaya ya asili katika njia ya kumfuata Yesu. Nendeni Galilaya ina maana ya jambo njema , likiwa na maana ya kugundua upya maana ya ubatizo wetu kama chemichemi ya maisha, ni kujenga nguvu mpya, kutoka vyanzo vya imani yetu na maisha yetu ya Kikristo . Kurudi Galilaya maana yake ni wote kurudi katika kuuona mwanga mkali wa neema ya Mungu, iliyonigusa mwanzo na kujiunga katika mwanzo wa safari ya wokovu. . Kutoka nguvu hiyo , nikaweza kuwasha moto wa imani unaomlika leo na kila siku , na kuleta joto na mwanga kwa ndugu zangu wake kwa waume. Kutoka mwali wa moto huo , mmezaliwa furaha wanyenyekevu, furaha isiyoweza kufadhaishwa na huzuni au dhiki, ila ni furaha nzuri , furaha ya upole.

Katika maisha ya kila Mkristo , baada ya ubatizo kuna pia Galilaya moja nzuri zaidi ya wa kukutana binafsi na Yesu Kristo ambaye aliyeniita kua mfuasi wake na kushiriki katika utume wake. Kwa maana hii, kurudi Galilaya inakuwa ni kumbukumbu ninayotakiwa kuiweka kama hazina ya thamani sana ndani ya kina cha moyo wangu , Yesu alipopita katika njia yangu, na kunitazama kwa huruma akaniomba kumfuata. Ina maana kufufua kumbukumbu ya wakati huo Wakati macho yake alikutana, wakati alipofanya mie nijisikie na kutambua kwamba ananipenda.

Papa alimalizia homilia yake akisema, , Usiku wa leo ,katika usiku huu, kila mmoja wetu anaweza kujiuliza , Je, ni ipi Galilaya yangu? Je, wakumbuka au umesahau? Je, limekwenda katika njia zilizonifanya kusahau Galilaya ?Basi na tumwombe Bwana , atupe msaada wa kukumbuka Galilaya yetu, kwa utambuzi kwamba, tunataka kurudi huko, kukutana na mwenyewe, aliyetuvutia kwa huruma yake.

Injili ya Pasaka ni wazi kabisa: tunahitaji kwenda huko , kumwona Yesu aliye fufuka , na kuwa mashahidi wa ufufuo wake. Hii si kurudi nyuma katika muda ; si aina ya kuchosha. Lakini ni kurudisha upendo wake kwetu kwa ajili ya kuupokea moto wa Yesu unaomulikia dunia na kuuleta mwanga huo kwa watu wote na hadi miisho yote ya dunia .
Galilaya ya mataifa (Mt 4:15; Isaya 8:23) ! Upeo wa Bwana Mfufuka, upeo wa Kanisa; hamu kali ya kukutana naye. Shime tushike mwendo wa kwenda Galilaya!
Katika Ibada hii, Papa alibatiza Wakatukumeni kumi, kati yao akiwemo mtoto wa miaka saba raia wa Italia na mtu mzima mwenye umri wa miaka 58 kutoka Vietnam. Wabatizwa wengine ni raia wa Ufaransa, Belarus, Lebanon na Senegal.








All the contents on this site are copyrighted ©.