2014-04-19 11:53:41

Baba Mtakatifu atoa zawadi ya Mayai ya Pasaka wa watoto waliolazwa Hospitali ya "Bambino Gesu"


Ijumaa Lori lililojaa mayai maalum ya kipindi cha Pasaka ambayo ndani yake yamejazwa chokoleti, moja kwa moja kutoka Vatican , lilipakua mzigo wake katika Hospitali ya Rufaa ya Watoto ya Bambino Gesù . Mayai hayo ni zawadi ya Papa Francisko kwa watoto waliolazwa katika hospitali hiyo, walau waweze kutoa tabasamu la kufurahia Siku Kuu ya Pasaka.
Shehena hiyo ya mayai makubwa yapatayo 150 ilitolewa kwa watoto waliolazwa katika idara ya Saratani.
Zawadi hii ni ishara ya mawazo mapya ya Papa Francisko kwa watoto wagonjwa katika hospitali hiyo ambayo aliitembelea wakati wa Mkesha wa Noeli mwaka jana 2013, Desemba 21. Baba Mtakatifu bado anaona hai moyoni mwake, tabasamu na kicheko cha watu siku hiyo alipopandisha katika hospitali hiyo iliyoko katika kilima cha Gianicolo, hapa Roma , ambako alizungukwa na kundi la waamini, Wauguzi na madaktari , wanaojihusika na utoaji wa huduma kwa watoto wadogo wagonjwa waliolazwa katika hospitali hiyo.
Hospitali hii ya jijini Roma, ni mali ya Jimbo la Papa tangu mwaka 1924, na inajulikana kama Hospitali ya Papa . Na Hospitali hiyo kwa mara ya kwanza iliwekwa katika uangalizi wa Papa Yohana XXIII, Na hivyo kuwa urithi wa Mapapa wote waliofuatia. Na Papa Francisko, Noeli iliyopita alirudisha utamaduni wa kutembelea watoto waliolazwa katika hospitali hiyo , inayojulikana kama Hospitali ya Papa.








All the contents on this site are copyrighted ©.