2014-04-17 11:35:00

Wasichana 100 kati ya 129 waliokuwa wametekwa nyara waachiwa huru!


Jeshi la Nigeria limefanikiwa kuwaokoa wasichana 100 kati ya 129 wa shule ya sekondari mjini Borno, Kaskazini mwa Nigeria waliokuwa wametekwa na Kikundi cha kigaidi cha Boko Haram, mapema juma hili. Taarifa zinaonesha kwamba, wasichana 14 walifanikiwa kujiokoa wenyewe kwa kuruka kutoka kwenye Lori lilikokuwa limewabeba.

Wasichana wengine 10 waliweza kutoroka wakiwa msituni, walipokuwa wameambiwa kuwapikia wanajeshi wa Boko Haram, na kuwaacha bila ya uangalizi makini. Taarifa ya kijeshi iliyotolewa na Meja Jenerali Chris Olukolade inasema kwamba, mwanajeshi mmoja wa kikundi cha Boko Haram ametiwa pingu, tayari kufikishwa mbele ya mkondo wa sheria.







All the contents on this site are copyrighted ©.