Serikali ya Cuba imeridhia kwamba, Ijumaa kuu, Siku ambayo Wakristo sehemu mbali mbali
za dunia wanakumbuka: mateso na kifo cha Yesu Kristo Msalabani, iwe ni Siku kuu ya
Kitaifa na kwamba, wananchi wa Cuba watapumzika. Uamuzi huu wa Serikali ulipitishwa
kwenye kikao cha Bunge, kilichofanyika mwezi Desemba, 2013.
Sheria hii itaanza
kutumika rasmi mwezi Juni, 2014, lakini kama ilivyotokea kunako Mwaka 2012 na Mwaka
2013 wananchi wa Cuba katika Siku kuu ya Ijumaa kuu kwa Mwaka huu watapumzika pia.