2014-04-16 10:01:40

Papa kuongoza Karamu ya Mwisho ya Bwana katika kituo cha Walemavu- Roma.


Baba Mtakatifu Francisko, Alhamis Kuu majira ya jioni, saa 11:30, ataadhimisha Karamu ya Mwisho ya Bwana, na liturujia ya kuosha miguu watu kadhaa kama ishara ya unyenyekevu na huduma, akiwa katika Kituo walemavu cha Shirika la Mtakatifu Maria wa Kudra ya Mungu, cha Shirika la la Don Gnocchi, cha mjini Roma. Shirika hili hufadhili watu wapatao elfu tatu wenye ulemavu na tegemezi nchini kote Italia, Rome kukiwa na vituo vyake 12 ambavyo hufadhili wageni wahitaji wanaoingia jiji la Roma, kati ya vituo vya 29 vinavyofanya kazi katika mikoa tisa ya Italia.

Baba Mtakatifu Francisko anasubiriwa kwa hamu na wagonjwa na familia zao katika cha kituo cha Mtakatifu Maria wa Kudra ya Mungu , mtaa wa Via Casal Marmo 401, Roma , ambako watu wa kujitolea huhudumia wagonjwa na familia zao. Alhamis Kuu ya mwaka jana Papa Francisko aliadhimisha pia Ibada ya Alhamis Kuu akiwa katika gereza la watoto la mjini Roma.
Kwa Alhamis Kuu hii, taarifa zinaeleza kwamba, tukio hili la Baba Mtakatifu, kukitembelea Kituo cha Waelmavu cha Don Gnocchi, linafanyika baada ya kupita wiki chache kwa shirika hili kuadhimisha sherehe kubwa ya kupita kwa miaka mitano tangu mwanzilishi wa shirika Don Gnocchi kutajwa Mwenye Heri Februari , sherehe iliyohudhuriwa na waelfu ya waamini, kama sehemu ya mipango kwa ajili ya maadhimisho ya miaka tano ya Don Carlo Gnocchi , kutajwa Mwenye Heri. Sherehe zilizo hamasisha mwamko mpya wa utamaduni wake wa muda mrefu na huduma maalum, isiyoweza kusahaulika, inayoonyesha kupandwa kwa Mbegu ya mshikamano na umoja kwa jirani katika utendaji wa Papa, " baba wa vilema ".

Kituo cha Mtakatifu Maria wa Kudra ya Mungu , ambacho zamani kilifanya kazi kwa jina la Mama Nasi, nyumba ndogo ya Maongozi ya Mungu ya Cottolengo, ilifanywa kuwa Shirika la Don Gnocchi Foundation Septemba 2003 na kwa sasa lina jumla ya 150 vitanda, ambamo kuna makazi kwa ajili ya huduma ya Afya kwa Watu wenye ulemavu 60 vitanda, ambao hawahitaji kuunganisha na vifaa vya aina hospitali au vituo vya ukarabati ); na pia kuna idara ya kisasa ya ukarabati wa mwili “ neuromotor” wa ngazi ya juu, wanaotumia vitanda 60 , ambao pia hupokea huduma ya mazoezi ya mwili, , huduma ya tiba , tathmini saidizi teknolojia na ushauri nasaha, nasaha za kisaikolojia na elimu kwa shughuli zinazo husiana na hali ya wagonjwa hao. Na vitanda 30 vilivyo baki , ni kwa ajili ya wanaotoa huduma kwa wagonjwa.

Mbali na huduma hiyo ya ndani pia huhudumia wagonjwa walemavu kama wagonjwa wa nje kila siku, ambao hupewa tiba na ushauri wa ukarabati na huduma za nyumbani .

Rais wa Shirika la Don Gnocchi, Mosinyori Angelo Bazzari , akizungumzia Papa Francisiko kuendesha Ibada ya Karamu ya Bwana katika kituo hicho cha Mtaa wa Via Casal Marmo , amesema ni furaha kubwa kwao na wanamkaribisha Baba Mtakatifu kwa furaha kubwa ndani mwao. Na kwamba, ishara ya kuosha miguu ni wazi inayoonyesha kwamba Kanisa tangu kuanzishwa kwake, daima limeitwa kuhudumia kwa unyenyekevu hasa watu masikini na dhaifu. Ni huduma ya upendo wa Papa katika ulimwengu wa mateso na ishara ya huruma ya Kiiinjili, ambayo husaidia kukumbuka kwamba , kiwango cha ustaarabu wa jamii kinapaswa kuwa kipimo katika uwezo wake wa kutembea pamoja na watu dhaifu.

Upendo huu wa kuhudumia dhaifu na wanyonge katika jamii, ni karama ya Don Gnocchi , aliyowaachia kama urithi wafanyakazi zaidi ya elfu tano wa Shirika lake, ambayo hufanya kazi kila siku kwa majitoleo ya bila kujibakiza , kwa uaminifu na kama msimamo kila siku , katika dhamira yao ya uwezo, nia, huduma na uendelezaji wa maisha ya maelfu ya watu wanaotafuta huduma katika vituo vya shirik, kwa ajili ya Utafiti wa Afya , mshikamano na huduma.








All the contents on this site are copyrighted ©.