Papa kuongoza Karamu ya Mwisho ya Bwana katika kituo cha Walemavu- Roma.
Baba Mtakatifu Francisko, Alhamis Kuu majira ya jioni, saa 11:30, ataadhimisha Karamu
ya Mwisho ya Bwana, na liturujia ya kuosha miguu watu kadhaa kama ishara ya unyenyekevu
na huduma, akiwa katika Kituo walemavu cha Shirika la Mtakatifu Maria wa Kudra ya
Mungu, cha Shirika la la Don Gnocchi, cha mjini Roma. Shirika hili hufadhili watu
wapatao elfu tatu wenye ulemavu na tegemezi nchini kote Italia, Rome kukiwa na
vituo vyake 12 ambavyo hufadhili wageni wahitaji wanaoingia jiji la Roma, kati
ya vituo vya 29 vinavyofanya kazi katika mikoa tisa ya Italia.
Baba Mtakatifu
Francisko anasubiriwa kwa hamu na wagonjwa na familia zao katika cha kituo cha Mtakatifu
Maria wa Kudra ya Mungu , mtaa wa Via Casal Marmo 401, Roma , ambako watu wa kujitolea
huhudumia wagonjwa na familia zao. Alhamis Kuu ya mwaka jana Papa Francisko aliadhimisha
pia Ibada ya Alhamis Kuu akiwa katika gereza la watoto la mjini Roma. Kwa Alhamis
Kuu hii, taarifa zinaeleza kwamba, tukio hili la Baba Mtakatifu, kukitembelea Kituo
cha Waelmavu cha Don Gnocchi, linafanyika baada ya kupita wiki chache kwa shirika
hili kuadhimisha sherehe kubwa ya kupita kwa miaka mitano tangu mwanzilishi wa shirika
Don Gnocchi kutajwa Mwenye Heri Februari , sherehe iliyohudhuriwa na waelfu ya waamini,
kama sehemu ya mipango kwa ajili ya maadhimisho ya miaka tano ya Don Carlo Gnocchi
, kutajwa Mwenye Heri. Sherehe zilizo hamasisha mwamko mpya wa utamaduni wake wa muda
mrefu na huduma maalum, isiyoweza kusahaulika, inayoonyesha kupandwa kwa Mbegu ya
mshikamano na umoja kwa jirani katika utendaji wa Papa, " baba wa vilema ".
Kituo
cha Mtakatifu Maria wa Kudra ya Mungu , ambacho zamani kilifanya kazi kwa jina la
Mama Nasi, nyumba ndogo ya Maongozi ya Mungu ya Cottolengo, ilifanywa kuwa Shirika
la Don Gnocchi Foundation Septemba 2003 na kwa sasa lina jumla ya 150 vitanda, ambamo
kuna makazi kwa ajili ya huduma ya Afya kwa Watu wenye ulemavu 60 vitanda, ambao
hawahitaji kuunganisha na vifaa vya aina hospitali au vituo vya ukarabati ); na pia
kuna idara ya kisasa ya ukarabati wa mwili “ neuromotor” wa ngazi ya juu, wanaotumia
vitanda 60 , ambao pia hupokea huduma ya mazoezi ya mwili, , huduma ya tiba , tathmini
saidizi teknolojia na ushauri nasaha, nasaha za kisaikolojia na elimu kwa shughuli
zinazo husiana na hali ya wagonjwa hao. Na vitanda 30 vilivyo baki , ni kwa ajili
ya wanaotoa huduma kwa wagonjwa.
Mbali na huduma hiyo ya ndani pia huhudumia
wagonjwa walemavu kama wagonjwa wa nje kila siku, ambao hupewa tiba na ushauri wa
ukarabati na huduma za nyumbani .
Rais wa Shirika la Don Gnocchi, Mosinyori
Angelo Bazzari , akizungumzia Papa Francisiko kuendesha Ibada ya Karamu ya Bwana
katika kituo hicho cha Mtaa wa Via Casal Marmo , amesema ni furaha kubwa kwao na wanamkaribisha
Baba Mtakatifu kwa furaha kubwa ndani mwao. Na kwamba, ishara ya kuosha miguu ni wazi
inayoonyesha kwamba Kanisa tangu kuanzishwa kwake, daima limeitwa kuhudumia kwa unyenyekevu
hasa watu masikini na dhaifu. Ni huduma ya upendo wa Papa katika ulimwengu wa mateso
na ishara ya huruma ya Kiiinjili, ambayo husaidia kukumbuka kwamba , kiwango cha
ustaarabu wa jamii kinapaswa kuwa kipimo katika uwezo wake wa kutembea pamoja na
watu dhaifu.
Upendo huu wa kuhudumia dhaifu na wanyonge katika jamii, ni karama
ya Don Gnocchi , aliyowaachia kama urithi wafanyakazi zaidi ya elfu tano wa Shirika
lake, ambayo hufanya kazi kila siku kwa majitoleo ya bila kujibakiza , kwa uaminifu
na kama msimamo kila siku , katika dhamira yao ya uwezo, nia, huduma na uendelezaji
wa maisha ya maelfu ya watu wanaotafuta huduma katika vituo vya shirik, kwa ajili
ya Utafiti wa Afya , mshikamano na huduma.