Wasi wasi wazuka Nigeria kuhusu matumizi ya silaha za kemikali
Jumuiya ya Kimataifa inaitaka Serikali ya Nigeria kufanya upembuzi yakinifu kuhusiana
na madai kwamba, katika mapambano Kaskazini mwa Nigeria imegundulika kwamba, kumekuwepo
pia na matumizi ya silaha za kemikali, kama ilivyoelezwa na Bwana Gabriel Suswam,
Gavana wa Jimbo la Benue, Nigeria wakati alipokuwa anatoa taarifa yake kwa Tume ya
ulinzi na usalama ya Seneti ya Nigeria hivi karibuni.
Matumizi ya silaha za
kemikali yasipodhibitiwa mapema anasema Gavana Suswam hakuna nchi jirani inayoweza
kuwa na uhakika wa usalama wa maisha ya raia wake. Nigeria inapaswa kuwahakikishia
wananchi wa Nigeria na Jumuiya ya Kimataifa kwamba, silaha za Kemikali zilizotumika
si kwa ajili ya maangamizi ya halaiki ya watu pamoja na kufahamu madhara yanayoweza
kusababishwa na matumizi ya silaha hizi kwa maisha ya watu.
Nigeria imetoa
ombi maalum kwa Umoja wa Mataifa kusaidia kufanya uchunguzi wa kina kuhusiana na madai
ya matumizi ya silaha za kemikali, Kaskazini mwa Nigeria.