2014-04-15 10:13:45

Maafa ya kutisha mjini Abuja!


Zaidi ya watu sabini na mmoja wamepoteza maisha na wengine mia moja na ishirini na wanne kujeruhiwa vibaya kutokana na mlipuko wa bomu uliotokea kwenye kituo kikuu cha Mabas, mjini Abuja, Nigeria, siku ya jumatatu, tarehe 14 Aprili 2014. Idadi ya watu waliofariki dunia inatarajiwa kuongezeka maradufu. Huu ni mwendelezo wa mashambulizi ya kigaidi yanayoitikisa Nigeria, licha ya mikakati ya Serikali kupambana na vitendo vya kigaidi vinavyoendeshwa na Kikundi cha Boko Haram nchini Nigeria.

Takwimu zinaonesha kwamba, tangu mwezi Januari hadi sasa kuna zaidi ya watu elfu moja na mia tano ambao wamekwisha poteza maisha kutokana na mashambulizi ya vitendo vya kigaidi, wengi wao ni raia wasiokuwa na hatia.







All the contents on this site are copyrighted ©.