Serikali ya Tanzania iko katika mchakato wa kuandaa Mkakati wa Kitaifa wa Ugharamiaji
Huduma za Afya ili kuhakikisha kila Mtanzania atapata huduma za afya za msingi bila
vipingamizi vyovyote vya kifedha. Hayo yalisemwa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dk. Seif Rashid wakati wa ufunguzi wa kukusanya maoni ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Huduma za Jamii kuhusu mkakati huo uliofanyika mjini Dodoma.
“
Serikali imedhamiria kuboresha utoaji wa huduma za afya, moja ya mkakati wa kufikia
malengo haya ni kuwa na mkakati endelevu… ninawaomba ushiriki wenu katika majadailiano
haya ili tuweze kutoka na mapendekezo yatakayoleta ustawi katika sekta ya afya na
hatimaye afya ya watanzania wote,” alisema Waziri.
Aidha Dk. Radhid alisema
licha ya uchangiaji wa huduma za afya kuanza rasmi mwaka 1993,ambapo wananchi walitakiwa
kuchangia baadhi ya gharama za afya katika vituo vya kutolea huduma vya umma kupitia
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, ulianzishwa mwaka 1999 na Mfuko wa Afya ya Jamii ulianza
mwaka 2001 na bima binafsi za afya kuaanzishwa.
“Pamoja na jitihada hizo, bado
rasilimali ni chache wananchi wanaopata huduma za afya kupitia mifuko mbalimbali ni
asilimia ni asilimia 18 tu ya Watanzania wote,” alisisitiza. Aliongeza kwamba,mkakati
huo unalenga kuongeza idadi ya watu watakaopata huduma za afya kwa kutumia mfumo wa
bima ili kuwahakikishia huduma wanazozihitaji. Hivi sasa gharama za matibabu ya afya
zimezidi kukua na zitaendelea kukua kuliko uwezo wa Serikali wa kutumia mapato ya
kodi.
Alizitaja baadhi ya sababu za kupanda gharama hizo ni taaluma kubadilika
kuwa za kisasa, madadiliko ya magonjwa, kuongezeka kwa magonjwa yasiyoyakuambukizana,
kuongezeka kwa idadi ya watu. Alisema ili kuendana na mabadiliko hayo ni muhimu kuwana
angalau hospitali ya rufaa moja kila mkoa, sita za wilaya, vituo vya afya 40 na zahanati
100. Alisema kutokana na hali bajeti ya kutosha inahitajika kila mwaka na kuwa na
njia bora ya kuhakikisha kila Mtanzania anakuwa na mfumo wa bima.
Kwa Upande
wake Kaimu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk. Donan Mmbando alisema takwimu zinaonesha
kuwa asilimia 33 ya Watanzania wanaishi katika hali duni ya umasikini. Alisema pia
takwimu zilizopo zinaonesha kuwa zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania hawana uhakika
wa kupata huduma za afya kwa sababu ya kutokuwa na mfumo mzuri wa kugharamia huduma
za afya hali inayosababisha baadhi ya magonjwa kuwa sugu.