Monsinyo Guido Marini kuendelea kuwa mshereheshaji wa Ibada za Kipapa
Baba Mtakatifu Francisko ameridhia uteuzi wa Monsinyo Guido Marini kuendelea kuwa
ni mshereheshaji wa Liturujia za Kipapa. Itakumbukwa kwamba, Monsinyo Marini aliteuliwa
na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi na sita, tarehe 1 Oktoba 2007 na amekuwa
akishiriki katika maandalizi na maadhimisho ya Liturujia na Ibada mbali mbali zinazoadhimishwa
na Baba Mtakatifu ndani na nje ya Vatican.
Monsinyo Guido Marini alizaliwa
kunako tarehe 31 Januari 1965 huko Genoa, Kaskazini mwa Italia.