2014-04-10 08:57:48

Kanisa linaomboleza kifo cha Askofu mkuu Boniface Lele


Askofu mkuu mstaafu Boniface Lele wa Jimbo kuu la Mombasa, Kenya amefariki dunia akiwa na umri wa miaka sitini na sita kutokana na ugonjwa wa shinikizo la damu. Askofu mkuu mstaafu Lele, Ijumaa tarehe 4 Aprili 2014 alilazwa Hospitalini Mombasa, akiwa na hali mbaya na tarehe 10 Aprili 2014 akafariki dunia kutokana na ugonjwa wa shinikizo la damu.

Kardinali John Njue, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya anasema, kifo cha Askofu mkuu mstaafu Boniface Lele wa Jimbo kuu la Mombasa ni pigo kubwa sana kwa Kanisa. Ni kiongozi aliyejitoa bila ya kujibakiza kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya Kanisa Jimbo Katoliki la Kitui na baadaye, Jimbo kuu la Mombasa. Ni kiongozi aliyekuwa mpole na mnyekevu, kweli atakumbukwa na wengi.

Kardinali Njue anawaalika waamini kumsindikiza Marehemu Askofu mkuu mstaafu Lele kwa sala na sadaka zao, ili aweze kupata pumziko la milele, miongoni mwa watakatifu wa Mungu. Familia ya Mungu Jimbo kuu la Mombasa, baada ya kupata taarifa hii ilikusanyika na kusali kwenye Hospitali ya Pandya, mahali ambako mwili wa Marehemu Askofu mkuu mstaafu Lele unahifadhiwa.







All the contents on this site are copyrighted ©.