Papa asikitishwa na watawa watatu kutekwa nyara Kaskazini mwa Cameroon
Baba Mtakatifu Francisko amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kutekwa nyara
kwa Mapadre wawili wa kutoka Jimbo Katoliki Vincenza, Kaskazini mwa Italia waliokuwa
wanafanya utume wao nchini Cameroon, kama Mapadre wa Zawadi ya Roho Mtakatifu, "Fidei
Donum" pamoja na mtawa mmoja kutoka Canada.
Baba Mtakatifu anaendelea kufuatilia
habari hizi kwa kuwasiliana na Ubalozi wa Vatican nchini Cameroon. Watawa hawa watatu
wametekwa nyara wakiwa kwenye makazi yao, Jimbo Katoliki la Maroua, Kaskazini mwa
Cameroon na Kikundi cha watu kinachosaidikiwa kuwa na uhusiano na Kikosi cha Kigaidi
cha Boko Haram.