2014-04-05 13:41:16

Maaskofu Katoliki Tanzania washiriki kwenye Njia ya Msalaba Kanisa kuu la Mtakatifu Yohane wa Laterano, Roma


Baba Mtakatifu Francisko, Jumamosi tarehe 5 Aprili 2014 amekutana na kuzungumza na Kundi la Pili la Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania linaloundwa na Jimbo kuu la Songea. Itakumbukwa kwamba, Kanisa la Tanzania linaundwa na Majimbo makuu matano yaani: Jimbo kuu la Dar es Salaam, Jimbo kuu la Tabora; majimbo yaliyoundwa kunako tarehe 23 Machi 1953. Askofu Marko Mihayo, akawa Askofu mkuu wa kwanza Tanzania kwa kupewa Jimbo kuu la Tabora. Majimbo makuu kuu ya Mwanza na Songea yaliundwa kunako Mwaka 1978 na Mwaka 1999 Jimbo kuu Katoliki Arusha likaundwa.

Maaskofu Katoliki kutoka Tanzania, Ijumaa jioni, wameshiriki kwenye Njia ya Msalaba kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Yohane wa Laterano, lililoko mjini Roma, ambalo pia ni Makao makuu ya Jimbo kuu la Roma.

Maaskofu wanasema, kwa kweli wanajisikia nyumbani kuzungumza na Baba Mtakatifu Francisko, kwani mtindo wake wa majadiliano unajikita katika maisha ya kijumuiya: kwa kuulizana, kushirikishana, kuhabarishana na kufafanuliana, ili kujenga na kuliimarisha Kanisa la Kristo nchini Tanzania, ili liweze kuwa kweli ni chombo cha kutangaza Injili ya Furaha. Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania linafanya hija ya kitume mjini Vatican kuanzia tarehe 4 hadi tarehe 7 Aprili 2014 kadiri ya ratiba elekezi. Maaskofu wafuatao wamekutana na kutetea na Baba Mtakatifu Francisko mjini Vatican Jumamosi tarehe 5 Aprili 2014.

* Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa, Askofu wa Jimbo Katoliki Iringa na Msimamizi wa Kitume, Jimbo kuu Songea.

* Askofu Bruno Pius Ngonyani, Jimbo Katoliki la Lindi

* Askofu Evaristo Marc Chengula, Jimbo Katoliki la Mbeya

* Askofu John Chrisostom Ndimbo, Jimbo Katoliki la Mbinga aliyeambatana na Askofu mstaafu Emmanuel A. Mapunda

* Askofu Gabriel Mmole, Jimbo Katoliki Mtwara

* Askofu Alfred Leonhard Maluma, Jimbo Katoliki Njombe

* Askofu Castor Paul Msemwa, Jimbo Katoliki Tunduru-Masasi

* Askofu Bernardin Mfumbusa, Jimbo Katoliki Kondoa

* Askofu Desiderius M. Rwoma, Jimbo Katoliki Bukoba na Msimamizi wa Kitume Jimbo Katoliki Singida.








All the contents on this site are copyrighted ©.