Tume yaanza utafiti katika mapitio ya mfumo wa sheria unaosimamia haki za walaji
Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania imeanza kufanya utafiti wa mfumo wa sheria unaosimamia
Haki za Walaji ili kubaini kasoro mbalimbali zilizoko kwenye mfumo husika na kupendekeza
njia sahihi ya kuboresha mfumo huo nchini Tanzania. Hatua ya Tume kufanya utafiti
huo inatokana na mendeleo ya sayansi, teknolojia pamoja na utandawazi ambayo kwa ujumla
yamemfanya mlaji kujikuta akiwa kwenye hatari ya kuathirika kiafya, kiuchumi na kijamii.
Tume katika utafiti wa awali, imebaini kuwa Mfumo uliopo hauendani na na wakati
huu wa mabadiliko ya kiuchumi, kijsamii, kitekenologia yanayotokea, kwani sheria nyingi
zilizopo zilitungwa muda mrefu na hivyo hazikuzingatia mahitaji ya wakati wa sasa.
Pia sheria nyingi hazijajumuishwa kwenye sheria moja zinasimamiwa na watu
au Taasisi tofauti tofauti. Hivyo, Tume imeona haja ya kupitia sheria hizo ili kupendekeza
mfumo wa sheria utakaomlinda mlaji kwa kuzingatia maendeleo yaliyopo sasa.
Na
ni matarajio yetu baada ya kukamilika kwa utafiti huu Tume tutakuja na mapendekezo
ambayo yataleta tija kwa walaji wetu pamoja na taifa kwa ujumla. Tume ya Kurekebisha
Sheria (Tume) ilianzishwa chini ya kifungu cha 3 cha Sheria ya Kurekebisha Sheria
Namba 11 ya mwaka 1980. Sheria hii kwa sasa ni Sura ya 171 ya Sheria za Tanzania Toleo
la Mwaka 2002. Tume ya Kurekebisha Sheria ni Idara ya Serikali inayojitegemea chini
ya Wizara ya Katiba na Sheria.