Malikia Elizabeth II akutana na kuzungumza na Papa Francisko mjini Vatican
Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi jioni tarehe 3 Aprili 2014 amekutana na kuzungumza
na Malkia Elizabeth wa pili wa Uingereza pamoja na ujumbe wake, waliopokelewa na Kardinali
Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican baada ya kumaliza ziara ya kikazi kwenye Ikulu
ya Italia. Mazungumzo kati ya Baba Mtakatifu na Malkia Elizabeth wa Pili anasema Padre
Federico Lombardi, Msemaji mkuu wa Vatican kwamba, yamedumu kwa takribani dakika ishirini.
Viongozi
hawa wawili wamebadilishana zawadi kama kielelezo cha kumbu kumbu yaziara ya Malikia
Elizabeth wa Pili mjini Vatican. Baada ya mazungumzo na Baba Mtakatifu Malkia Elizabeth
alirejea tena London, Uingereza. Hii ilikuwa ni ziara ya masaa machache lakini yenye
umuhimu mkubwa katika kudumisha ushirikiano wa kimataifa.