2014-04-02 15:45:39

Dunia yawakumbuka Watoto wenye wigo wa akili (autism)


Tarehe 2 Aprili , ni siku ya kuwakumbuka watoto wenye ulemavu au wigo wa akili . Hili ni adhimisho la saba la Dunia kwa ajili ya watoto hao.
Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya kazi za Kichungaji kwa Wafanyakazi na wahudumu wa Afya, Askofu Mkuu Zygmunt Zimowski, ameiadhmisha siku hii kwa na wito wa kuejnga matumaini na ushirikiano wa dhati na familia au wale wote waliojitolea kuishi na watoto wenye ulemavu wa akili. Na kwamba, katika maadhimisho ya Siku hili, Dunia inaonyesha huruma na na upendo wa kina kwa watoto hao, na hivyo inakuwa ni changamoto kwa Kanisa zima kuishi ukweli wa upendo wa Kristo kwa watu wote wakiwemo atu wenye matatizo ya wigo wa akili. Askofu Mkuu Zimowski, amehimiza wasiokuwa namatatizo hayo katika familia zao, kuw ana moyo wa huruma majitoleo ya sadaka ya kutoa msaada hasa wa huduma, ili wale wanaowatunza pia wapate muda wa kufanya shughuli nyingine.
Amesema familia zenye kuwa na watoto hawa walemavu wa akili wanastahili kupata msaada wa mawazo pia na kihali, na hasa pale panapokuwa na hisia za kukata tamaa au uwepo wa mgogoro katika mahusiano na hisia kwamba tatizo hilo linatokana na muungano wao katika uzazi. Ni hali ngumu halisi, inayo hitaji ushirikiano na mawasiliano na uelewa na hekima kwa familia zenye matatizo haya.Na wapo wengi wanaokubali hali kama mpango wa Mungu.
Hivyo amesisitiza Askofu Mkuu Zimowski, ni muhimu kupambana na unyanyapaa wa aina yoyote , hasa kupitia njia ya ushirikiano katika jamii, kuvunja vizuizi na kutengwa, na chuki zinazo tokana na uwepo wa mgonjwa huyo, badala yake iwe ni kuimarisha uhusiano, hasa kati ya wazazi. Na pia inaweza kufanikisha msaada wa utendaji wa jamii katika mazingira ya huduma, habari, mawasiliano na mafunzo, kuwezesha kwa njia hii ya mpito kwa ufahamu wa kweli na kukubalika kwa ugonjwa huo, ambayo kukanusha na kukemea hali yoyote iliyotaka kudhoofisha hadhi ya mgonjwa.

Hivyo, inawezekana kuanzisha misingi ya matumaini kwa kutowatenga watu wenye ugonjwa wa akili , au familia zao, ikilishwa na mizizi ya umoja, kushirikiana na kuaminiana katika mshikamano adilifu wa kijamii. Na kwamba, mkazo mkubwa wa Kanisa, ni kuunga mkono na kuhamasisha matumaini mapya katika uwanja wa matatizo ya wigo wa akili .

Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya kazi za Kichungaji kwa wafanyakazi na wahudumu wa afya, katika adhimisho la siku hii, ametangaza kwamba, mkutano wa kimataifa wa XXIX , utakao fanyika Novemba 20-22 ijayo na Baraza, watakuwa na mkutano huo mjini Vatican, kwa ajili ya kushughulikia mada: "Matatizo ya wigo wa akili : uwepo wa Tumaini.







All the contents on this site are copyrighted ©.