2014-03-31 16:08:13

Papa awahimiza Wasalesiani kuwaendea vijana wanyonge katika jamii


(Vatican Radio)Jumatatu 31 March 2014, majira ya asubuhi, Baba Mtakatifu Francisko, alikutana na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa 27 wa Shirika la Wasalesiani wa Don Bosco, na kutoa shukurani zake za dhati kwa Mkuu wa Shirika, Padre Angel Fernandez Artime, na pia kwa wanashirika wote . Alionyesha imani yake kwa uongozi wa shirika linavyo tembea katika njia yake. Na aliwaombea Roho Mtakatifu, awawezesha kuelewa matarajio yao na changamoto za wakati wetu, hasa kwa vijana, katika tafsiri ya mwanga wa Injili na Karama zao, katika misingi ya majiundo ya utume wa Shirika. .

Hotuba ya Papa, ilirejea madhari ya mkutano “kuwa Mashahidi Jasiri Injili" kama daima, ilivyokuwa nia ya mtangulizi wao , Don Bosco, ambaye alisisitiza mawili : kazi na kiasi. Kazi na kiasi hivyo unakuwa ni mhimili wa shirika. Papa alieleza na kuasa dhidi ya mwelekeo wa kufikiri na kufanya kazi kwa faida binafsi, na kuanguka katika majaribu ya kidunia. Alikumbusha utendaji wote wa shirika iwe kwa ajili ya Mambo ya Mungu na Ufalme wake. Kisha kiasi iwe katika hisia za uwiano wa maisha ya kawaida kwa wanashirika, wakimulikiwa na umaskini wa Don Bosco na Mama Margaret, katika kuona umuhimu wa maisha ya msalesiani katika misingi ya maisha ya ila binadamu , na hasa katika kuwa karibu na maskini, uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa mali .


Aidha Papa alizungumzia Uinjilishaji wa vijana katika utume wa Roho Mtakatifu iliyekabidhiwa kwa Kanisa, katika maana ya uhusiano wa karibu na vijana na elimu yao, wakilenga kutembea pamoja katika safari ya kukua katika imani Kiinjili, na ukomavu wa kibinadamu. Papa amezungumzia haja ya kuwaandaa vijana kufanya kazi katika umoja wa roho ya Injili , kama mawakala wa haki na amani, na kuishi katika mshikamano na viongozi wao na wakuu wa Kanisa. Na alitaja hili linahiji jambo la kwanza kabisa , sala, ndipo shughuli za pamoja , na kisha , mipango ya kibinafsi na ujasiri wa kutoa mapendekezo na kusindikizana katika maisha ya ushirika kama familia moja ya Wasesiani. Kujali pia mahitaji mpya msingi kwa ajili ya majiundo, elimu uongozi na utambuzi.

Na amewahimiza Wasalesiani, zaidi kuwaendea na kufanya kazi na vijana, wanaoonekana kusahaulika au kupuuzwa na jamii kutokana na hali yao duni ya kimaisha. Vijana walio jitenga au kutengwa. Papa amewaalika kuzifikiria hali halisi, hasa tatizo kubwa la ukosefu wa ajira, na matokeo yake hasi. Na pia kufikiria juu ya utegemezi , ambayo kwa bahati mbaya,anasema mizizi yake inatokana na ukosefu wa upendo wa kweli. Na kuwafikia vijana waliowekwa pembezoni , kunahitaji ujasiri katika sala, maombi , ukomavu binadamu na mahusiano ya kweli. Na kwamba kuna umuhimu wa vijana hawa kuendelea kusindikizwa mara kwa mara.

Na Papa alimshukuru Mungu kwa uwepo wao na kwa kufanya kazi zao, ambazo huzifanya si kama mtu binafsi, lakini kama jumuiya, wakidumisha kila utendaji wa kitume katika karama za mwanzishi wao . Na ameasa dhidi ya hatari za mivutano ya ndani am bayo hasa misingi yake ni ubinafsi , akiomba waione haja ya kuwa mawasiliano ya kina na mahusiano halisi miongoni mwao. Na kwa nguvu ya kuimwilisha Injili, wataweza kuishi kwa udugu aliishi, kuheshimiana, kusaidiana , kuelewana , kutendeana kwa wema, msamaha na furaha . Roho wa familia Don Bosco wanayorithi , ni msaada mkubwa katika maana ya kuwa na moyo uvumilivu na ujenzi wa ubunifu katika maisha yaliyowekwa wakfu.
Na aliwatakia kila la heri kwa ajili ya maadhimisho ya kutimia miaka mia mbili ya kuzaliwa kwa Don Bosco.Pia aliwaombea msaada wa Mama Maria , Msaada wa Wakristo, ambaye hajawahi kushindwa kutoa misaada yake, kwa wanaomkimbilia.Kwa Maombezi yake ya kimama, Mungu hutoa matunda yanayotarajiwa. Na aliwapa Baraka zake za Kipapa, na kuwaomba wamwobee pia.








All the contents on this site are copyrighted ©.