2014-03-31 12:24:46

Kwaresima ni kipindi cha kubadili mwelekeo wa maisha!


Kwaresima ni kipindi na mwaliko wa toba, wongofu wa ndani, sala na tafakari ya kina ya Neno la Mungu, linalomwilishwa katika huduma ya mapendo kwa jirani. Ni kipindi cha kukimbilia huruma na upendo wa Mungu kwa njia ya Sakramenti ya Upatanisho, inayomwonjesha mwamini ile furaha, huruma na upendo wa Baba ambaye daima anasubiri kuwaona watoto wake waliokimbia kutoka nyumbani, wakirejea kwa toba na unyenyekevu wa moyo!

Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anasema, kwamba, Kwaresima ni kipindi cha kubadilisha mwelekeo wa maisha, kwa kupambana kufa na kupona na ubaya pamoja na umaskini wa maisha ya kiroho, kihali na kipato.







All the contents on this site are copyrighted ©.